http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumatatu, 20 Oktoba 2014

SNP GWAJIMA: IBADA YA JUMAPILI SOMO: SHERIA MBILI ZA ROHONI

SOMO: SHERIA MBILI ZA ROHONI
TAREHE: 19/10/2014
NA MCHUNGAJI KIONGOZI: JOSEPHAT GWAJIMA


 























Kuna ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili. Mtu anapofanikiwa rohoni baadae anafanikiwa mwilini. Inaweza kuwa magonjwa au ukawa na matatizo yakikutokea mwilini jua kuwa yameanzia rohoni. Unapoanza kuomba na kushambulia lazima utambue kuwa unashindana na ulimwengu wa roho.Imeandikwa;
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Waefeso 6:12
Kumbe kabla ya kubarikiwa lazima ubarikiwe rohoni. Tukizungumzia miji ya kiroho, inamaana kwamba ulimwengu wa roho ni sawa na miji unayoiona hapa duniani. Ukiona watu wanajua maneno au mistari ya biblia yote, sio ishara ya kuwa yeye anauwezo wa kuyajua yote na namna ya kushindana. Mungu ni roho, hivyo lazima tumwabudu katika roho. Imeandikwa.
Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; Yohane2:24
Viumbe katika ulimwengu wa roho mfano, Mungu, malaika, mashetani
Viumbe wa kimwili ni kama wanadamu, kuku, simba, miti
Katika ulimwengu wa roho, kuna sheria mbili zinazouongoza. Mambo yote huanzia katika ulimwengu wa roho, hasa katika ndoto. Zipo sheria 2, zinazoongoza ulimwengu wa roho.
1. KUBADILIKA UMBO NA KUVAA UMBO LOLOTE
Ili mashetani ambao ni wachawi ili waweze kwenda kuroga lazima watoke ndani ya miili yao na kuvaa umbo jingine. Kwa kuwa anakuwa rohoni anaweza kuvaa umbo lolote, na kugeuka kuwa kitu chochote. Mfano, paka, mbwa, kunguru. Lakini wachawi wanaposikia hukutambua kuwa ni wachawi wanafurahi sana. Imeandikwa; Marko 16:12
12 Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba.
Yesu aliwatokea wanafunzi wake akiwa na sura nyingine, lakini kwa kuwa alikuwa rohoni, alionekana kuwa na sura nyingine. Yesu anasura nyingine, kama umezoea kumuona daktari leo anasura nyingine, akitaka kukutokea kama mmea natakutokea kama ua la sharoni, au mzee wa siku, lazima utambue kuwa laizima atokee kwa sura nyingine.
Ukiri; leo katika jina la yesu yesu akutokee kwa sura nyingine, kama umezoa yesu ni mponyaji tu leo anasura nyingine, ni mfariji, ni mfalme wa wafalme, ni mwamba wa kale. Leo lazima yesu atokee kwa sura nyingine sawa na tatizo ulilonalo. Amen.
Yesu aliamua kubadili sura lakini wanafunzi wake walijua ni yeye. Kila unapoongezeka kila hatua unaongeza marafi unaongeza maadui pia. Lakini kama ulikuwa umezoea kutembea kama chura tambua kuwa unatakiwa kuruka juu kama tai. Imeandikwa;……………………………. Yohana20;15
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
Nirahisi sana watu kukuamini lakini mtu aliyekuzoea hawezi kukuamini kirahisi, ndiyo maana Yesu alimtokea mama yake kwa sura nyingine kama mtunza bustani, ili aweze kumwamini. Watu wamemzoea yesu wa kuponya magonjwa tu lakini yesu anatokea kwa sura nyingine ili mambo yaweze kutokea na kumwamini.
Hivyo ili uweze kufanya ya rohoni lazima uvae sura nyingine. Imeandikwa; ufunuo 1:9
9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.
10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,
Roho inaweza kuvaa sura yoyote ndiyo maana Yesu alimtokea Yohane katika sura nyingine kwenye kisiwa cha Patmo.. Imeandikwa;
Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari. Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, Mwanzo18; 1-2
Kumbe roho inaweza kugeuka na kuwa kitu chochote, na kufanaya kazi kama wanadamu. Imeandikwa;
Huwafanya malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa moto wa miali. zaburi 104:4
Ukishaona matukio kama hayo unahisi ni upepo kumbe kuna watu ndani ya upepo. Unaweza kuona upepo unakuja ukahisi ni upepo kumbe ni mjomba au bibi yuko ndani ya upepo. Lazima utambue kuwa kuna upepo unaosumbua hali ya maisha yako ndo maana unaona taabu na misukosuko.
Yesu alisema na tuvuke ng’ambo ya pili lakini shetani aliyajua hayo na kutikisa chombo. Tambua hata wewe kwenye maisha yako ukiona umepanga kufanya jambo lolote la maendeleo na mara gafla matatizo yanaanza usikubali pigana maana ni upepo huo umetengenezwa ili usifike unakoenda au usifanye unachotaka kufanya. Imeandikwa;
Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.
12 Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao. Kutoka 7; 11-12
UKIRI
Kuanzia leo kila atakae jigeuza kwa sura yoyote nitamuona kwa Jina la Yesu.
Haimanishi kuwa mashetani wanaouwezo wa kutengeneza chura, au nyoka au fimbo ila tu waliweza kunuizia kitu kikageuka na kutimiza lengo. Malaika anaweza kufanya vile hata mashetani wanaweza kuvaa sura na maumbo ya kitu na kutimiza kusudi. Imeandikwa;
Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.2Wakoritho 11:14
AINA NNE ZA MASHETANI
1. Majoka amabao ni roho ya uovu walioanguka kutoka mbinguni baada ya uasi. Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; Ufunuo 12;7
2. Mizimu. Haya ni mashetani waliotawala ukoo kwa muda mrefu.
3. Miungu. Ni mashetani waliopewa makafara kwa muda mrefu na wakapewa nguvu na kuwa miungu
4. Majini. Hawa nai mashetani wenye asili ya kiarabu.
Imeandikwa;
Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. Ufunuo 16:13
Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza; Ufunuo 18:2
Nguvu kubwa ya mashetani ni ule uwezo wa kutowatambua. Wanapotoka ndani huwa wananuiza na kuvaa maumbo bandia. Wachawi nao huwa wanasikiliza kama umewatambua, wakiona umeona visivyo wanafurahi maana wanajua kuna biashara inaendelea na wamefanikiwa.
Ukiri.
Kuanzia leo lazima kila atakekuja kuniroga nitamuona kwa jina la Yesu.Kila aliyegeuza umbo naamuru nimuone katika umbo lake la siri.
Watu wengine wanajisikia kama wana misumari ndani ya miili yao lakini jambo amabalo hukulijua kama limetengenezwa an kugeuka kuwa kisu ndani ya miili yao. Ukiona nchi inayumbayumba lazima ujue kuna chanzo chake kiko katika ulimwengu wa roho. Ukishinda rohoni unaweza kuua kwa siraha isiyorasmi .
Yawezekana umeumwa sana na hujui namna ya kutatua tatizo ulilonalo.Imeandikwa;
Inawezekana, unajisikia hali mbaya hasa ya kumtukana mume wako, au mke wako lakini kwa akili zako huwezi kusema vile, lakini ukajikuta unasema vile. Kimsingi kuna viumbe wa rohoni wanakaa ndani yako ndo maana wakati mwingine unajikuta umeshatukana.
Inawezekana, unaona uso wako unaweka makeup, lakini sura iko kama babu, jambo usilolijua ni kuwa yuko aliyetumwa na kugeuka na kuwa babu.
MAOMBI
jini, joka, mzimu, aliyegeuka umbo na kuja kwangu, lazima nikuone katika jina la yesu.nina waamuru wapigwe katiak jina la yesu.Mimi ni askari naangusha ngome za balaa, ngome za mikosi, ngome za magonjwa katika jina la Yesu. Mimi nakataa kutawaliwa katika jina la yesu.
Kuanzia sasa roho yoyote iliyogeuka na kuwa balaa, talaka, mikosi, magonjwa, naivunja katika jina la yesu. Kwa jina la yesu kuanzia leo chochote kilichotumwa, nilichikinunua, nakiangamiza katika jin layesu. Kitu chochote, au roho yoyote, iliyondani ya nyumba yangu naivunja, na irudisha ilikotoka katika jina la Yesu.
Kwa jina la yesu,
2. UNAMFUMBA MTU ASIKUTAMBUE.
Katika sheria mbili za rohoni pili ni kukufumba usimtambue, na wewe ukiona unahisi ni vitu hivyo ulivyoviona kwa macho au katika ndoto. Akili ya mtu akifungwa mtu akiona hatambui kama ni wachawi au mashetani. Yawezeka kila ukilala na kuota ndoto ukiamka unaanza kusema uliyoyaota ambayo yako katika sura bandia. Inatakiwa uwafunge ili wasijifiche wakija uwatambuae katika jina la Yesu. Omba maombi haya kwa jina la Yesu. Maana imeandikwa Imeandikwa ;
Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya Yohana 14:13-14
MAOMBI
Katika jina la yesu namteketeza mtu yeyote aliyejigeuza sura ili anitese namfyeka katika jina la yesu.
Kila atakaekuja katika umbo lolote lazima nimjue katika jina la Yesu, ninawafunga wasinitambue kama nimewaona. Kuanzia leo naamka toka usingizi wa kiroho, na akili yangu iwaze kutawala, iwaze biashara katika jina la Yesu . Kuanzia leo naanza kutambua kazi yangu, nianze kuelewa kazi ya kufanya, biashara ya kufanya, katika jina la Yesu.
Nawashambulia mashetani wote katika jina la Yesu, mashetani walioshikiria familia yangu, kazi yangu, ndoa yangu, biashara yangu katika jina la Yesu nawaangamiza katika jina la Yesu. Nawaangamiza maadui wote katika jina la Yes. Natumia mamlaka aliyonipa Yesu nawafyeka wanaozuia kazi yangu nawafyeka wanaozuia ndoa yangu, nawafyeka wanaozuia huduma yangu, katika jina la Yesu. Nawashambulia kwa damu ya mwanakondoo.
Imeandikwa;
Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana. Isaya 54:17
Nawafyeka katika jina la Yesu, mtu yeyote aliyesimama kwenye njia zangu kunizuia nisifanikiwe, kuzuia nisisonge mbele kunizuia nisipate ajira, nafunga uwezo wako wa kujigeuza na kuwa balaa, nakujigeuza kuwa mikosi, kuwa matatizo ,kuwa mtego na balaa, nawashambulia katika jina la Yesu.
Naharibu uwezo wenu katika jina la Yesu, ng’oa madhabahu zenu katika jina la Yesu. Nawatiisha, na kata mamlaka zenu, kaila kiumbe kinachotumia mazira kuharibu maisha yangu nawashambulia katila jina la Yesu. Naaribu uweza wenu wote katika jina la Yesu.
Natangua yote uliyoyapanga katika jina la Yesu. Imeandikwa; yeye uyatangua mashauri ya wadanganyifu na mikono yao isipate kutimiza makusudi yao.
Kila vibarua wa shetani mnaovaa sura bandia nawaangamiza katika jina la Yesu, navunja kila laana ya familia iliyonipata kupitia viumbe wa rohoni mnaojibadilisha sura na kuniroga nawafyeka katika jina la Yesu.
Kila nguvu ya giza inayotawala nailaani katika jina la Yesu, kila balaa zinazotawala nazivunja katika jina la Yesu. Nakiri leo niko huru, kazi yangu iko huru katiaka jina la Yesu. AMEN
Inua mikono juu; na ukiri maneno haya kwa nguvu
Kila jini aliye ndani yangu uliyeingia ili mimi nisiolewe, ili uniletee balaa, imeandikwa lolote mtakalolifunga hapa duniani , litafungwa na mbinguni ewe jini uliyetumwa ofisini kutoka kijijini, nakuapisha dhihirika na ujulikane kwa jina la Yesu. Jini makata, jini wa hasira, jini wa mikosi, kila aliyerogwa kwa kuwekewa dawa kwenye tumbo la uzazi, kwenye maji ya kuoga, kwenye chakula, kwenye kitanda, kwenye nguo, kwenye damu wakati wa siku zangu naamuru moto ndani yangu ukuunguze na unitoke katika jina la Yesu.
-----------------------------------AMEN---------------------------------------------

Jumatatu, 13 Oktoba 2014

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA-

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 12/10/2014

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA

SOMO: HAIKUWA HIVYO TANGU ZAMANI

Utangulizi
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima

 Kanisa leo limefanywa kuwa mahali pa kukutania baada ya uchovu wa wiki nzima. Lakini haikuwa hivyo tangu zamani; kanisa lilianzishwa kama mahali pa kutatua matatizo yaliyoshindikana ndani ya wiki nzima.
“Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha katika tumaini;
Kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote  pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” Warumi 8:19-22

Kumbe kuna viumbe ambavyo vimebebeshwa utumwa wa aina fulani ambavyo vinategemea kuwekwa huru.
Ulimwengu tunaouendea utakuwa ni ulimwengu ambao sio wa kushinda kwa sababu ndugu yako ni mbunge, waziri ama raisi, bali utakuwa ni ulimwengu wa kushinda mambo yote kwa imani. Tunakiendea kizazi ambacho mwenye haki ataishi kwa imani.

“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” Mwanzo1:28
Haya ni mamlaka ambayo Mungu alimpa mwanadamu zamani sana kabla nyumba hazijajengwa, kabla  mavazi hayajaanza kutengenezwa. Kwanza ni kuzaa na kuongezeka iwe mwilini au rohoni. Pili ni kutiisha kila kitu kwenye nchi; mapori, majangwa, milima. Tatu, kutawala kila kitu angani, baharini na nchi kavu. Hivi ndivyo ilivyokuwa tangu mwanzo, asili yetu kama wana wa Mungu ni kutawala sio kutawaliwa. Lakini leo wana wa Mungu wamekuwa watu wakuogopaogopa; sivyo ilivyokuwa. Tuliumbwa kutiisha na kutawala angani, baharini na kwenye nchi.
Mungu ni Mungu wa kusema. Kabla hajatenda huwa anaongea kwanza. Ndio maana biblia nzima imejaa ahadi za Mungu, anasema atatubariki, atatuinua. Hivyo inatupasa  na sisi kuongea na kuikiri asili yetu. Tunatawala kwa mujibu wa sheria ya kitabu cha Mwanzo ibara ya kwanza kifungu cha ishirini na nane. Biblia ni sheria ya Bwana wa Majeshi na sheria hii haiwezi kubadilika kizazi hata kizazi.

Kwa asili ya mwanadamu alitakiwa atawale majini, angani na katika nchi. Shetani alipoona mwanadamu amepewa mamlaka hiyo akamfuata Adamu ili aibe mamlaka hiyo. Kwa kuwa sisi nasi tulikuwa katika viuno vya Adamu wakati anatenda dhambi iliyomgharimu mamlaka yake tumehesabiwa dhambi kutoka kwake..
“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

Ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tama za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili nay a nia, tukawa kwa tabi yetu watoto wa hasira kama na hao wengine” Waefeso 2:1-3
Ndio maana leo shetani anaitwa mkuu wa anga. Kabla ya Adamu na Eva hawajatenda dhambi walikuwa wanatiisha anga, nchi na bahari. Walipokosea walipoteza mamlaka yao ambayo ilichukuliwa na shetani. Shetani aliichukua anga na kuitawala ndio maana akaitwa mfalme wa anga.
“Nao wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hwakupenda maisha yao hata kufa.
Kwa hiyo shangilieni enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wan chi na bahari! Kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache.” Ufunuo12:11-2
Adamu alikuwa anamiliki anga, bahari na nchi. Shetani alipofanikiwa kumtoa Adam, akafanikiwa kumiliki vyote alivyokuwa anamiliki. Ndio maana sasa kuzimu ina sehemu kuu tatu; angani, baharini na kwenye nchi.
Kama wana wa Mungu ambao tunatakiwa kuishi kwa imani ili kumpendeza Mungu;  kutamka, kusema na kukiri ahadi za Mungu kabla hazijawa bayana katika ulimwengu wa mwili ni sehemu ya maisha yetu. Tamka kwa bidii yaliyomo ndani ya moyo wako kwa maana uweza wa uzima na mauti u ndani ya kinywa chako. Hii ndiyo imani itupasayo kuishi kwayo. Imani ina viwango vinne;

Ø Unachowaza
Awazavyo mtu moyoni mwake ndivyo alivyo. Ni muhimu kujua namna ya kuyatiisha mawazo yako ili yawe sawasawa na namna ambavyo Mungu anawaza kuhusu wewe.

Ø Unachosema
Chochote uwazacho baada ya muda fulani utakikiri kwa kuwa hii ndiyo asili yetu kutoka kwa Mungu; kusema kabla jambo halijatokea.

Ø Unachotenda
  Ukishawaza na kukiri ni lazima uanze kutenda kuelekea kwenye lile jambo ambalo unaloliamini.

Ø Tendo la Imani
Hili ni tendo ambalo unatenda ambalo huwa ni kinyume na hali halisi ya mambo katika ulimwengu wa mwili.
Pasipo Imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Mungu ni Mungu wa makusudi, hivyo lazima ufahamu kusudi lako katika maisha. Maendeleo hayaji kwa kuota utakuwa unatembea ukaokota mamilioni ya fedha halafu ukafanikiwa, mafanikio yoyote huja kwa hatua za kuhifadhi kidogokidogo kile ulicho nacho. Pale ambapo kusudi lisipofahamika matumizi mabaya lazima yatokee.

Hivyo shetani alipomtoa Adamu kwenye utawala akakaa yeye kuwa mtawala wa anga, nchi, bahari na vyote vilivyomo. Kabla Adamu hajatenda dhambi, akiwa bado ni mtawala; sisi tulikuwa ndani ya viuno vyake hivyo tulionja utawala huo. Baada ya shetani kuuchukua utawala kutoka kwetu, ana uwezo wa kuvitiisha viumbe vyote baharini, angani na kwenye nchi. Anayo mamlaka ya kuamuru viumbe kama bacteria, virusi , protozoa kuingia ndani ya miili ya wanadamu na kusababisha magonjwa au hata mauti. Leo dunia ina kila aina ya magonjwa na nyuma ya kila ugonjwa kuna kiumbe. Lakini viumbe hivi vimetiishwa kwa ubatili na yule aibaye ambaye ameiba mamlaka yetu. Haikuwa hivyo tangu zamani.
Mwanzoni Adamu hakuwa na magonjwa kabisa kwasababu alikuwa anatawala anga na viumbe vyake vyote, nchi na viumbe vyake vyote bahari na viumbe vyake vyote. Hivyo viumbe vyote vilikuwa chini ya utiisho wake. Hii ndiyo asili ya mwanzo ya mwanadamu.
Kwa nini leo kila janga kubwa linatokea Afrika? Vita vya kikabila, siasa mbovu, umaskini uliopitiliza, magonjwa ya ajabu; ukimwi unaua sana Afrika, ebola, mafua ya ndege, mafua ya nguruwe, dengue. Ni nini kinatokea? Shetani hawapendi waafrika kwa sababu anajua kutokea kwao ndipo utakapotokea ule uamsho wa siku za mwisho utakaogeuza tawala zote kuwa tawala za mwanakondoo. Imani bado ipo Afrika.
Tangu mwanzo shetani amekuwa akiona dalili za Afrika kuwa jeshi la mwisho la Mungu ndio maana anainua vita juu yake. Wana wa Israeli waliishi Afrika kwa miaka mia nne na thelathini utumwani Misri, miujiza mingi ilitokea Afrika  kule Misri. Haitoshi  alipozaliwa Yesu, malaika alimtokea Yusufu akamwambia amchukue Mariamu mkewe na mtoto Yesu na kuwapeleka katika nchi ya Misri. Wakati wa kubeba msalaba, ilipofika hatua  Yesu hawezi kuubeba tena alitokea Simon mkrene (Krene ni Afrika mahali panapoitwa Libya leo.) akaubeba msalaba mpaka Kalvari. Hii ni kuonyesha kuwa injili ya siku za mwisho itabebwa na waafrika. Ndio maana biblia inasema kutakuwepo na madhabahu katika nchi ya Afrika ( Isaya 19:4) 4 Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, Bwana wa majeshi.
Yesu alivyokuja duniani alikuja kuturudishia utawala wetu ulioibiwa na shetani. Basi kumbe leo shetani anatawala isivyo halali, sisi ndio watawala halali. Tunayo mamlaka ya kuvitiisha viumbe vyote viletavyo magonjwa  kukaa nje ya mipaka ya Tanzania kwa jina la Yesu na vikatii.
Ebola ni mpango wa kuzimu, ni hukumu ya kifo kwa waafrika ili kuipunguza nguvu yetu. Na sisi kama watawala leo tumegundua asili yetu na hila ya yule alaye. Hivyo inatupasa kuchukua hatua kama watawala kutiisha, kumiliki na kutawala.
 
 
Maelfu ya watu wakiomba ndani ya bonde la kukata maneno

MAOMBI.
Ninaamuru kama mtawala wa bakteria, virusi na viumbe vyote wa magonjwa hamna uwezo juu yangu kwa jina la Yesu. Hamna mamlaka juu ya Tanzania. Ninawatiisha viumbe wote wanaoonekana na wasioonekana wasababishao magonjwa kwa jina la Yesu, hamtaingia ndani ya Tanzania kwa jina la Yesu. Kwa mamlaka niliyonayo ninawafunga virusi wote wa mafua ya ndege, virusi wa mafua ya nguruwe, ebola  nje ya Tanzania kwa damu ya Yesu. Kemikali zote, bakteria, protozoa wote ninawatiisha kwa damu ya Yesu Kristo. Kwa mamlaka ya damu ya mwanakondoo, viumbe wote wa magonjwa ninaupiga ule uweza uliowekwa ndani yenu juu ya Tanzania, juu ya Afrika, juu ya maisha yangu, juu ya familia yangu; ninaamuru kuanzia sasa  hamtaingia ndani ya nchi ya Tanzania kwa jina la Yesu.Ninavimiliki na kuvitiisha viumbe vyote vinavyokaa kwenye anga, bahari, na nchi. Mimi ni mtawala wenu, hamna mamlaka ya kunitawala  haikuwa hivyo tangu zamani. Ninawaseta mrudi kuzimu mlikotoka kwa jina la Yesu. Ninaamuru kuanzia sasa hamtanidhuru kwa damu ya Yesu. Viumbe vyote vinavyoonekana na visivyoonekana hamna uwezo wa kunitawala kwa jina la Yesu Kristo. Ninabeba mamlaka kama mtawala, ninawateketeza na uwezo wenu wa kudhuru kwa damu ya mwanakondoo. Nimepewa amri juu ya pepo wachafu na viumbe vyote, ninaangamiza kila nguvu iliyo juu yenu ninyi viumbe wa kishetani na kichawi na waganga wa kienyeji, ninawakausha kwa damu ya Yesu Kristo. Niwaondolea ule uwezo wa kuidhuru Tanzania kwa mamlaka ya damu ya mwanakondoo. Ninaiachilia damu ya mwanakondoo kwenye mipaka yote ya Tanzania,  damu inenayo  mema, ninainyunyizia kwenye mipaka yote ya Taifa la Tanzania na juu ya watu wake wote. Iwalinde dhidi ya magonjwa yote kwa jina la Yesu. Kwa mamlaka ya Jina la Yesu kristo ninatawala viumbe vvyote  vilivyomo baharini,  angani na kwenye nchi kwa damu ya Yesu. Ninatawala uchumi wa nchi, utajiri wa nchi; ninautawala kwa jina la Yesu Kristo. Ninatawala kwa jina la Yesu Kristo, ninatawala na kuvitiisha viumbe vyote vya magonjwa kwa jina la Yesu Kristo. AMEN!