http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumanne, 20 Mei 2014

INGEKUWA BONGO INGEKUAJE? AFUNGWA MIAKA 17 KIMAKOSA

Miaka 17 jela kwa kosa ambalo hakufanya

Victor Nealon
Mwanamume aliyefungwa jela kwa miaka kumi na saba kimakosa ameombwa radhi nchini Uingereza.
Mwanamume huyo alihukumiwa jela baada ya mahakama kumpata na hatia ya kosa la kujaribu kumbaka mwanamke ingawa tume ya kuchunguza kesi za watu waliofungwa jela kimakosa imemuomba radhi.
Victor Nealon, 53, alihukumiwa kwa kosa la kumshambulia mwanamke nje ya ukumbi wa densi mwaka 1996.
Aliomba tume ya kuchunguza kesi za wafungwa waliohukumiwa kimakosa kuchunguza kesi yake ingawa alipuuzwa mara mbili.
Hukumu yake ilifutiliwa mbali mwaka jana.
Tume hiyo sasa imesema ilipaswa kuchunguza kesi yake kwa umaakini ingawa hilo halikufanyika.
Mwenyekiti wa tume hiyo Richard Foster amenukuliwa akisema: "ninajuta sana kwa sababu kuna jambo fulani katika kesi hii ambalo hatukulichunguza vyema, tunamuomba radhi mwathiriwa. ''
'kukosa kuchunguza'
Bwana Nealon, ambaye siku zote alikana madai ya njama ya kumbaka mwanamke , alikamatwa baada ya mwanamke kudai kuwa mwanamume huyo alimdhulumu kimapenzi akiwa anarejea nyumbani kutoka klabuni katika mtaa wa Redditch.
Mtuhumiwa alifungwa jela baada ya mahakama kumpata na hatia na kumhukumu maisha jela.
Alisema kuwa alitaka tume hiyo kuchunguza ushahidi wote uliotolewa katika kesi hiyo.
Mawakili wake hata hivyo ndio waliochunguza ushahidi huo na kupata chembechembe za DNA ambazo sio zake bali za mtu asiyejulikana na kukosoa polisi kwa kuficha ushahidi huo.
Hukumu yake hatimaye ilifutiliwa mbali mwaka 2013.
Alisema: 'Ningekuwa nimeondoka jela miaka kumi au kumi na miwili iliyopita lakini kutokana na kosa la tume kukosa kuchunguza kesi yangu, ilinibidi kuhudumia kifungo kwa kosa ambalo sikufanya.''

bbc

Jumatatu, 19 Mei 2014

MCHUNGAJI GWAJIMA AFUNDISHA SOMO LA MADHABAHU YA UHARIBIFU

Jumapili Mei 18, 2014

Na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, 18 Mei 2014.





1. 0 Utangulizi

Maandiko ya Msingi: Zaburi 18: 1-50, Waamuzi 6:1-40, 

Kipindi ambacho Taifa la Israel walipokuwa watumwa wa wamidian, watu walikuwa wanaonewa sana na kunyang’anywa mali zao hata mazao yao yalikuwa yakiharibiwa. Hivyo Gidion alikuwa amejificha kwenye mwamba akipepeta ngano ndipo malaika akamwita ewe shujaa Gidion,,lakini Gidion alikataa kuitwa shujaa kwa maaana alikuwa hajiamini. Lakini malaika akamhakikishia kuwa yeye ni shujaa ila ile madhabahu ya Baali aliyokuwa nayo baba yake ndiyo iliyokuwa inamshikilia hata asijitambue kuwa ni shujaa. Hii inatufundisha kuwa kuna madhabahu mahali ambayo inakuzuia wewe usifanikiwe kama Mungu alivyokusudia kwako.

Kwenye madhabahu ile ya nyumbani kwao Gidion kulikuwapo na ashera pia, ashera ni mti uliopandwa kwa ajili ya kusimamia kitu fulani , kwa mfano mti unaweza kupandwa kwa jina la mtu na ule mti ukistawi ndipo mtu Yule anapata matatizo mfano ugonjwa ndiyo maana kuna mtu anakuwa mgonjwa wakati wa masika hii ni kwa sababu ya ule mti unakuwa umenawili kwa mvua. Kuna mtu yuko mahali hapa na watu wasiompenda wamempandia mti eidha wa balaa, magonjwa, umasikini, kukataliwa, kuachwa na kadhalika, lakini leo tunatuma radi na kulipua maashera yote kwa jina la Yesu.

Kwa hiyo Gidion akaambiwa na bwana wewe ni shujaa unatakiwa kwenda kupigana vita ila kwanza bomoa madhabahu iliyo kwenye mji huu inayofanya watu kuwa waoga. Na sisi leo watu wa Ufufuo na Uzima tunaenda kila mahali ilipo madhabahu inayolishikilia Taifa letu na tunaibomoa kwa jina la Yesu. Leo lazima watu wote waliolazwa kwenye madhabahu ya nchi hii watatoka na kuelekea  katika hatima zao na mafanikio yao kwa jina la Yesu.  Gidion baada ya kuibomoa madhabahu ya Baali  watu wa mji walimtafuta ili wamwuue lakini baba yake Gidion (Yoashi) akasema mwacheni baali ajitetee mwenyewe kwa kubomolewa madhabahu yake, kwa hiyo nakutangazia hata wewe leo hakuna dhara hata moja litakalokupata kwa kuzibomoa madhabahu za wachawi .

2.0 MADHABAHU NDANI YA BIBLIA

Mwanzo 8:20, Nuhu alipotoka kwenye safina akamjengea Mungu madhabahu, Hii inaonyesha kuwa kila madhabahu lazima iwe na tukio inaloliwakilisha, kwa mfano kuna madhabahu za utawala, kwa hiyo huwezi kumwondoa mtawala aliye na madhabahu imara mpaka uibomoe ile madhabahu ndipo uguse utawala wake.  Mwanzo 12:7, Ibrahim alipoongea na bwana kwamba nchi ile amepewa ndipo alipojenga madhabahu mahali pale ili isimamie umiliki wake aliopewa kwenye  ile nchi, ndiyo maana hata sasa hakuna mtu anayeweza kuwanyang’anya wa Israel nchi yao ingawa mataifa mengi wamejaribu kuwaondoa lakini wameshindwa. Mwanzo 12:8, 13:14, Utaona watu kwenye biblia walikuwa wakijenga madhabahu mahali ili  isimamie jambo fulani.

Madhabahu ni mahali ambapo wachawi na waganga wa kienyeji  wanakusanyikia , wanapokuwa mahali pale wanatoa kafara za damu na wanakuja na mashitaka ya kuwashitaki watu na wananza kujadili. Kwa hiyo mchawi mmoja anapeleka shitaka la kumshitaki mtu kwa mfano atasema simpendi fulani kwa sababu analinga eti anahela ,au ana watoto wasomi au anapendwa sana na watu hivyo  nataka tumkomeshe. Kwa hiyo wachawi wanasema sawa tutamkomesha na ndipo wanapoanza kumtumia mtu mashetani ya kumharibia maisha yake.  Lakini leo nakutangazia kuwa madhabahu zote zilizotesa maisha yako lazima zibomolewe kwa jina la Yesu.  Ninayo ndoto  na ndoto yangu ni kuwa Falme za dunia zimekuwa Falme za mwanakondoo na hii imeishakuwa kwa maana madhabahu za kichawi zilizozuia injili ya Yesu zitabomolewa zote kwa jina la Yesu.

Mchawi anapenda kumshambulia na kumwuua mtu wa karibu yake kwa mfano kaka, dada, mama, baba nakadhalika. Kwa mfano mtu anataka dada fulani asiolewe kabisa, anapeleka jina lake kwenye madhabahu na kumwaga kafara, kwa hiyo kuanzia pale yule dada hawezi kuolewa kabisa kwa maana madhabahu inakuwa inaongea fulani asiolewe, asiolewe. Mwingine anaweza kuwekwa kwenye madhabahu ya uoga, kwa hiyo hawezi kufanya lolote kwa kuogopa eidha hasara kama ni biashara, ajali kama ni safari, kuachwa kama ni ndoa nakadhalika.

Madhabahu inaweza kuwa kakiwanja fulani ambapo wachawi wanakutanikia na kutoa kafara za damu kwa miungu wao. Mtu anaposhitakiwa na jina lake kutajwa mahali pale ndipo mashetani yanaanza kumwandama na kumharibia mambo yake, kwa hiyo mtu yule hawezi kufanikiwa hata afanyeje mpaka atakapoibomoa ile madhabahu. Madhabahu zinapobomolewa watu wanaachiliwa kwa hiyo wachawi na waganga wa kienyeji wanapata hasara, ndiyo maana Gidion alitafutwa auawe kwa kuibomoa madhabahu ya baali iliyokuwa nyumbani kwa baba yake Yoashi. Leo tutabomoa madhabahu iliyokutesa na kuwalaza  kwenye hiyo madhabahu wale waliokuwa wamekulaza kwa jina la Yesu.

Madhabahu /kiwanja cha wachawi huwezi kukiona kwa macho lakini kipo na wachawi wanakutana pale kila usiku na kuwashitaki watu. Ndiyo maana utaona watu wengi wana matatizo yasiyoisha, kwa mfano kuna mtu amelazwa kwenye madhabahu ya kuachwa kwenye ndoa kwa hiyo utamwona mama ameshaolewa na wanaume watatu nakuachwa na wote bila sababu ya msingi.

Mungu anapotaka kumwinua mtu anaruhusu apitie mambo magumu sana kila upande na asione msaada. Ndipo sasa mtu anapoona hana msaada anakumbuka kumlilia Mungu. Kwa mfano Israel walipokuwa na njaa kali sana mpaka watu wamefikia hatua ya  kula watoto wao, ndipo Mfalme akasema mwambie nabii Elisha kesho saa saba atakatwa kichwa asipotabiri kwa habari ya njaa kwenye taifa la Israel. Baada ya kutishwa ndipo nabii Elisha alitoa unabii kwamba kesho chakula kitapatikana tena kwa bei nafuu sana kuliko hata kabla ya njaa kutokeaa na  kesho yake yakatokea kama vile Elisha alivyosema. Hii inafundisha kuwa mtu unapopata matatizo usianze kulia wala kuwalaumu watu bali wakati huo ni wakatiwa kuutafuta uso wa Mungu ili upate jibu la kukutoa mahali pale.  Usifikiri magumu yanayokupata Mungu amekuacha siyo ni kwamba Mungu anataka uanze kumlilia na kumtafuta yeye kwa moyo wako wote kwa maana aliona umeanza kwenda mbali naye.
Kwa hiyo kuna madhabahu ambayo inaweza kuwa imemshikilia mtu mfano mtu anaweza kuwa amelazwa kwenye madhabahu ya umasikini hata akisoma na kusafiri nchi zote duniani hawezi kufanikiwa. Kwa hiyo ili mtu huyo afanikiwa lazima aibomoea ile madhabahu. Leo kila mtu ataomba kulingana na udhaifu alio nao kwenye maisha yake kwa mfano mtu mwenye hofu ataomba akisema kwa jina la Yesu naibomoa  madhabahu ya hofu iliyonishikilia na kuiharibu kafara waliyoitoa kwenye hiyo madhabahu.   Kwa jina la Yesu leo naamuka na kuondoka kwenye madhabhu walioyonilaza kwa jina la Yesu. Na mtu yeyote aliyepeleka jina langu kwenye madhabahu  hiyo namponda kwa jina la Yesu.

Wakati mwingine madhabahu inaweza kuwa siyo kiwanja bali inakuwa kwenye kitu chochote kile, kwa mfano dada mmoja alikuwa anafanya kazi kwenye kampuni ya tajiri, siku moja yule dada akaingia kwenye ofisi ya boss wake na kuona chupa ndogo lakini ndani ya ile chupa yumo yule dada akiwa hai. Hii inatufundisha kuwa yule dada alikuwa amelazwa kwenye madhabahu ya yule tajiri , kwa hiyo mafanikio aliyonayo yule tajiri ni kupitia nyota ya yule dada. 

3.0 MAMLAKA TULIYOPEWA NA BWANA WETU YESU KRISTO
Mathayo 10:1, kwa hiyo watu wa Mungu tumepewa mamlaka ya kutamka na ikawa na leo tunaenda kuzibomoa madhabahu zote kwa jina la Yesu. Mambo hapa dunia hayatokei yenyewe ila kuna kitu  kinafanywa ili yatokee. Na nguvu ya kufanya mambo yatokee ni uwezo wa mtu wa Rohoni  alionao ndiyo unaleta matokeo mazuri ya mwilini. Kwenye ulimwengu wa Roho unapotamka kwamba navunja madhabahu iliyonishikilia mahali popote itakuwa kama utakanyotamka.

4.0 HITIMISHO
4.1 MAOMBI
Kwa damu ya mwanakondoo naibomoa madhabahu ya wachawi kwa jina la Yesu, mahali popote walipotaja jina langu napaharibu kwa jina la Yesu, Naibomoa hali ya  kuwa kichaa, naibomoa madhabahu ya wendawazimu,naibomoa madhabahu ya mikosi kwa jina la Yesu. Mtu yeyote aliyenilaza kwenye madhabahu yake ya utawala leo naondoka na nakataa kubaki pale kwa jina la Yesu na nyota yangu naimuru ianze kung’aa.

Nakataa watoto wangu , kazi yangu, ukoo wangu kuwekwa kwenye madhabahu ya wachawi kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu ya kifo, umasikini,uoga na mikosi kwa jina la Yesu. Imeandikwa Gidion aliwapeleka watumishi wake kumi wakaibomoa madhabahu ya baali, na sisi watumishi wa Mungu leo tunazibomoa madhabahu zote zilizoshikilia taifa letu na watu  kwa jina la Yesu.  Imeandikwa bomoeni bomoeni hadi msingini, leo nabomoa madhabahu zote, madhabahu ya dhiki, magonjwa, umasikini kwa jina la Yesu. Nabomoa madhabahu ya shaba, udongo, chuma ,mti kwa jina la Yesu. Nakataa kushikiliwa kwa jina la Yesu, mtu yeyote anayenicontrol kupitia madhabahu yoyote leo nakaataa kwa jina la Yesu. Madhabahu ya mabaya iliyoimarishwa naivunja kwa jina la Yesu, mabaya hayatanipata mimi. Naamuru mizimu, majini, majoka anza kuondoka kwa maana madhabahu zenu zimebomolewa kwa jina la Yesu.  Imeandikwa bwana amenifunga mshipi wa vita,  leo nafanya vita na kuziteketeza madhabahu zote na nawachinja makuhani wote wa hizo madhabahu.

Naivunja madhabahu inayoninyima promosheni,inayonizuia nisisafari, inayonizuia nizipate pesa kwa jina la Yesu,.  Na kuhani yeyote aliyenipeleka kwenye hizo madhabahu leo namchinja . Imeandikwa bomoeni bomoeni hadi msingi leo naenda kubomoa madhabahu za njia panda, porini, bahari . Nainyamazisha damu iliyomwagwa kwenye madhabahu za wachawi kwa damu ya Yesu. Ninaamuru kuanzia sasa kila madhabahu inayonena nainyamazisha kwa jina la Yesu. Kila madhabahu iliyojengwa kwenye nchi ya Tanzania ili kukamata akili na nia za watanzania leo nakupasua vipanda vipande kwa jina la Yesu. Naamru na roho zote zilizolazwa kwenye madhabahu zianzae kuamka kwa jina la Yesu. Nakata kamba zote zinazounganisha watu na madhabahu za wachawi kwa jina la Yesu.

Nakata ashera zote zilizopandwa kwa majina ya watu kwa jina la Yesu. Nazilaani ashera zote na kuanzia sasa zianze kukauka kwa jinala Yesu. Nawateka nyara wasimamizi na makuhani wa madhabahu  nawachinja kwa jina la Yesu. Ewe Mungu wa madhabahu nakukamata na kukuteketeza kabisa na enzi yako yote kwa jina la Yesu. Leo naamuru mioyo, nafsi, akili na vyote vilivyoshikiliwa kuachiliwa kwa jina la Yesu. Nauzima moto uliwashwa kwenye madhabahu ya wachawi ili watu wapate magonjwa, kichaa, umasikini , balaa na mikosi kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu iliyojengwa kwenye kichwa, tumbo, kifua  kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu iliyohai na inayotembea kwa jina la Yesu.

Ufunuo 6:9, kuna roho za watu zinaweza kuwa zimewekwa chini ya madhabahu.  Hata wewe leo unaweza kuwa hapa lakini roho yako imelazwa kwenye madhabahu, sema leo naivunja madhabahu iliyonilaza na toka kwa jina la Yesu. Wachawi wa familia wanaweza kumwuuza mtu na kumpeleka alazwe kwenye madhabahu.  Leo naiteketeza hati ya makubaliano yao ambayo imewekwa kwa jina la Yesu, hati iliyonifanya niuzwe na nibaki madhabahuni leo naichana na kuiteketeza kabisa kwa kwa jina la Yesu.


Alhamisi, 15 Mei 2014

SNP JOSEPHAT GWAJIMA: IBADA YA JUMAPILI MEI 11, 2014. SOMO: VITA VYA HALI

JUMAPILI AMBAYO UTUKUFU WA MUNGU ULIJIDHIHIRISHA KWA NGUVU KATIKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA KAWE-Dar es Salaam

SOMO: VITA VYA HALI
PASTOR: SENIOR PASTOR JOSEPHAT GWAJIMA
11th May 2014 , Sunday
  
 Zaburi 27:1-14, Vita vya hali ni somo linaloendana na somo la matukio ya kichawi 
Ayubu1:19-24, Kuna vita vya hali kwa mfano mtu anaweza kusikia uchungu, au hali ya hewa na mazingira kwa mfano watoto wa Ayubu waliuawa na hali ya hewa ya upepo mkali . Ibilisi aliporuhusiwa na Mungu kugusa maisha ya Ayubu na tukio mojawapo alilolitenda ni kuanza kuleta hali mbalimbali ili kusudi watu wajue kuwa ni matukio ya hali ya hewa, shetani alileta upepo tokea pande nne ukaipiga nyumba na watoto wa Ayubu wakafa. Rusifa anasababisha hali ikiwa ni mojawapo ya silaha za kuwashambulia watu. Leo tunataka tushindane na vita ya hali kwa jina la Yesu, Wanadamu wengi hawajui kuwa shetani anatumia hali ya kushambulia maisha yao, kwa mfano hali ya moto, mvua kali, upepo , hali ya mtu kujisikia Uchungu, hali ya kukosa amani nguvu nakadhalika.
Leo tunatangaza kila silaha ya kukosa amani , kila silaha ya woga na kila silaha ya hali itakayofanyika juu yako wewe haitafanikiwa kwa jina la Yesu.  Kwa mfano tulipokuwa Ubungo kila siku nikitaka kuhubiri wingu linatanda na mvua inanyesha na mimi mhubiri nalowana  na baada ya kugundua kuwa ni hali ya vita  kwa hiyo nikaanza kufunga anga kabla ya kuanza ibada.
Kuna matukio yanatangazwa kwenye vyombo vya habari kama maafa ama majanga ambayo yametukia kutokana na hali mbalimbali lakini watu wanapokea taarifa hizo bila kujua kuwa ni matukio ya kichawi yanayoletwa na hali.
Kuna hali ya kuharibika biashara yako iliyotengenezwa, hali ya kuachwa, hali ya kuumwa na hali mbalimbali zinazotengenezwa kinyume na maisha ya mtu. Leo tunaenda kushindana kwa maana imeandikwa kwa maana kushindana kwetu siyo juu ya damu na nyama bali juu ya falme mamlaka wakuu wa giza na majeshi ya pepo wachafu. Je hayo mafuriko ni kawaida, siyo  hiyo ni vita vya hali ya hewa ya mvua, maana imeandikwa katika ufunuo  “joka akafunua mdomo na mto ukatoka ili kumgarikisha mtu, unaona joka alitoa mto , kumbe shetani anaweza kutoa mto na kugharikisha watu.  Kwa hiyo mtu anaweza kutengenezewa hali ya hewa ya joto na akawasha AC mpaka akachoka lakini joto liko palepale.
Kumbe shetani anaweza kunyoosha mkono wake na hali fulani ikampata mtu, kwa mfano mtu anaweza kutengenezewa hali ya kutokutulia mpaka ukimwuliza hawezi hata kuelezea hali yake.  Utaona shetani alitengeneza moto ukatoka mbinguni na kuteketeza kundi la wanyama wa Ayubu.
Freemasons ni wakala wa shetani na wamepewa uwezo wa kutengeneza hali mbalimbali  juu ya mtu kwa mfano  wanakuwa na makongamano ya kuzibadilisha fikra za watu hii ina maana wanatengeneza hali fulani ndani  mtu  ili aamini kuwa mafanikio yanaweza kuja  bila uwezo wa Mungu. Watu wanaingizwa kwenye freemonson society kwa kuvutwa na wenzao ,kwa kukaribishwa na kuambiwa maneno ya kutiwa moyo, kupewa zawadi na kusaidiana kumbe huo ni mtego. Utasikia mtu anaambiwa kuwa kuna Society inayoitwa Global Brotherhood inayosaidia watu kubadilisha mtazamo na fikra za mtu kuelekea mafanikio makubwa. Hakuna kitu hapa duniani kinachoweza kutokea chenyewe. Na duniani kuna makundi ya watu watatu:
      I.           kundi la kwanza wasiojua kinachoendelea na  watu hawa ni kundi kubwa na wanaweza kuitwa wapumbavu/ wajinga .
         II.            kundi la pili ni wale wanaojua kinachoendelea  lakini hawajui  jinsi ya kutenda kwenye hilo wanalojua.
     III.            Kundi la tatu ni wale wanaojua kinachoendelea na wanajua la kutenda kwenye hilo ninaloendelea hawa ni wachache sana na wanaitwa wenye hekima/akili.

Uchawi una makundi matatu
·         Black magic – hawa ni wachawi wanaoruka na kula nyama za watu na uchawi huu ufanyika kwa siri.
·         White magic -- uchawi uliokubalika na jamii na ukitendwa watu wanaona hauna madhara mfano wanamazingaombwe
·         Black Science - wanaweza kutengeneza virusi  vya magonjwa na wakatupa kwa watu, wanaweza kutengeneza hali ya hewa fulani mfano matetemeko, mvua kubwa nk.
Vifaa hizi vya hali ya hewa vinatengenezwa sehemu mbalimbali hata wajapani wengi wanatengeneza vifaa hivyo. Hata kwenye biblia utaona Musa alipoyapiga maji kwa fimbo yake ukatokea upepo mkali na bahari ikagawanyika , hiyo ulikuwa silaha ya hali.  Leo nakutangazia kwa jina la Yesu kuwa hakuna silaha ya hali ambayo itafanyika juu yako na kufanikiwa kwa jina la Yesu.
Black science ni watu waliochukuliwa msukuleni na huko wanakutana na mashetani na wanaanza kuwafundisha technologia ya kuonekana kwa macho na  hali ya hewa ni mojawapo ya hizo technologia.kwa mfao Japani wametengeneza Train inayokwenda underground kwa kasi sana 500km kwa saa na haina dereva inaendeshwa electronically , lakini ukiwauliza mmetoa wapi hii technologia hawajui ilikotokea , lakini hii inaonyesha kuwa mpinga Kristo analeta technologia hizi kuuleta ulimwengu pamoja ili aweze kutawala vizuri wakati wake ukifika.
Hali mbalimbali zinaweza kutengenezwa kwa mfano ndege kubwa yenye watu mia nne ikapotea kabisa , utajiuliza imekwenda wapi? Hii ni hali imetengenezwa na ndege  ikachukuliwa  na kuyeyushwa kabisa, hii inadhibitisha kuwa ufalme wa giza unatenda kazi nyuma ya matukio. Nyakati hizi ni za kuwa makini sana kwa maana shetani anatembea katikati ya watu na anajiungamanisha na wanadamu. Kila mtu mchana wa leo aliyetengenezewa hali fulani kwa mfano hali ya ugonjwa, hali ya umasikini, hali ya kukataliwa nk na mtu ametulia na kuridhika leo nakutangazia kuwa Mungu anataka utoke kwenye hali hiyo kwa jina la Yesu. Kuna watu wengine wametengenezewa hali ya kutojikubali , mtu anajisikia unyonge kila wakati mpaka anaogopa kuwa kati kati ya watu wengine.
 
MAOMBI
Kwa jina la Yesu hali niliyowekewa ya kukataa ndoa, hali ya kuogopa, hali ya kujikataa, hali ya kuwashwa naikataa kwa jina la Yesu, nami leo navaa hali ya ujasiri na kuzishambulia hali za kishetani zinazonisumbua  kwa jina la Yesu. Nawasha moto na kuteketeza hali ya maumivu inayonisumbua, hali ya kukosa usingizi na hofu wakati wa usiku , hali ya kujiona mnyonge na kujiona sifai, nayaamuru mapepo yanayohusika na hali hizo yang’oke na kuniachia  kwa jina la Yesu.
Katika jina la Yesu kuanzia sasa nasimama kinyume na hali  yoyote ya kishetani  iliyonipata, nasimama kinyume na silaha ya hali iliyonipata kwa jina la Yesu. Nasambaratisha hali ya aibu iliyonipata, hali ya kupata hasara kwenye biashara, hali ya ugonjwa na udhaifu kwa jina la Yesu. Nakataa hali ya umasikini, hali ya unyonge, hali ya kuonewa, hali ya magonjwa, hali ya aibu, hali ya kushindwa kwa jina la Yesu. Nawasambaratisha mashetani wote wanaonifuatilia na kuniletea hali mbaya kwenye maisha yangu kwa jina la Yesu. Imeandikwa kila silaha itakayofanyika juu yangu haitofanikiwa, naamuru silaha zote za kuniletea hali mbaya zivunjike kwa jina la YESU. Imeandikwa kila pando asilopanda baba yangu wa mbinguni litang’olewa, nang’oa hali ya huzuni mliyonipandia, nang’oa hali ya uchungu mlionipandia kwa jina la Yesu. Enyi mashetani mnaovaa sura za watu na sura za hali mbalimbali  na kuja kunitesa leo nawaamuru kudhihirika  na kutoweka kabisa kwenye maisha yangu kwa jina la Yesu.
 
CHANZO: GCTC
 **********************************AMEN************************************

Nigeria yapuuza matakwa ya Boko Haram

 
Nigeria yapuuza Boko Haram

Rais wa Nigeria ametupilia mbali matakwa ya la kundi la kiislam la Boko Haram kwamba serikali iwaachilie huru wafungwa wa kundi hilo ndipo litawachilia wasichana zaidi ya 200 waliiotekwa na kundi hilo.
Serikali ya Nigeria imesema iko tayari kwa mazungumzo na kundi la wanamgambo la Boko Haram.
Hata hivyo, inaendelea kubainika kuwa kuna mipaka ambayo serikali inaaishiria kuwa haitavuka.
Kwa mujibu wa waziri wa Uingereza anayehusika na masuala ya Afrika, Mark Simmonds aliye ziarani nchini Nigeria, Rais Goodluck Jonathan amemwambia wazi kuwa serikali haitakubali pendekezo la Boko Haram kubadilishana wafuasi wake waliofungwa jela na serikali na wasichana waliotekwa nyara na kundi hilo.
Lakini hilo ndio sharti pekee ambalo kiongozi wa Boko Haram, Abubacar Shekau ametoa.
Nigeria yapuuza matakwa ya Boko Haram kabla ya kuwaachilia wasichana.

Haijulikani sasa mazungumzo kati ya serikali na kundi hilo yatahusu nini baada ya pande zote mbili kushikilia misimamo mikali.
Waziri huyo wa Uingereza amesema baada ya mzozo uliopo kutatuliwa kuna haja ya kuwajibisha waliotekeleza utekaji nyara huo ambao ni , Abubacar Shekau na wafuasi wa Boko Haram.
Tamko hilo pia linaongezea uzito katika msimamo wa serikali na hivyo kutilia shaka uwezekano wa mzozo huo kutatuliwa kwa haraka.

bbc