http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Ijumaa, 27 Septemba 2013

Wakuu wa usalama kuhojiwa Kenya

Sehemu ya jengo la Westgate iliyoporomoka
Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.
Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.

Walipuuza onyo?

Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

source: bbc

Alhamisi, 19 Septemba 2013

GOLI 6 ZA SIMBA ZAWAINGIZIA SH.MIL.13.8




MIL 58/- ZAPATIKANA MECHI YA SIMBA, MGAMBO
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

MIKATABA YA MAKOCHA VPL, FDL YATAKIWA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Ijumaa, 6 Septemba 2013

ALIYEZIMIA MIAKA 19 AZINDUKA, HAELEWI KINACHOENDELEA


MTU mmoja aliyepata ajali na kuzimia kwa miaka 19 ameamka katika uzingizi wake na kujikuta akishangaa nini kinaendelea duniani.
Mtu huyo raia wa Poland alizimika wakati chama cha kikomunisti kipo madarakani na siasa ya ujamaa ikitawala na kuamka chama hicho kikiwa hakipo madarakani na ujamaa ukiwa umekufa.
Wakati anazimika chakula na umeme vilikuwa vikipatikana kwa resheni na kuamka kila mtu akiw abize kusaka chakula manake serikali haitoi tena wala haigawi kwa mfumo wa kila mtu awe nacho japo kidogo.
Televisheni ya Poland ilimuonesha mfanyakazi huyo wa zamani wa reli Jan Grzebski, 65, akielezea kushangaa kwake na mabadiliko aliyoyakuta baada ya kuamka.
Inadaiwa kwamba aligongwa na treni mwaka 1988.
Anaamini kuamka kwake kunatokana na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo mkewe Getruda ambaye alikuwa anamhudumia kipindi chote cha yeye kuwa usingizini. Madaktari walisema kwamba nafasi ya kuishi kwa mtu huyo ni miaka miwili au mitatu tu.
Alisema kuamka kwake kumemfanya aone mabadiliko mengi na hasa kujaa kwa vituj madukani, watu wanatamba na simu za mikononi njiani hali inayomfanya aone kizunguzungu .
"Now I see people on the streets with mobile phones and there are so many goods in the shops it makes my head spin," he told Polish television.
A comatose patient is in a profound state of unconsciousness which renders them unaware of both self and the world around them, and from which they cannot be roused.
Although those in a coma do not respond to stimuli in a meaningful way, contrary to popular belief they do not always lie quiet and still - in some cases they can move, open their eyes and even talk.
Fall of communists
"It was Gertruda that saved me, and I'll never forget it," Mr Grzebski told news channel TVN24 of his recovery.
Mrs Grzebski is reported to have moved her husband every hour to prevent bed sores.
"I cried a lot, and I prayed a lot," Mrs Grzebski said on Polsat television.
"Those who came to see us kept asking: 'When is he going to die?' But he's not dead."
When Mr Grzebski had his accident Poland was still ruled by its last communist leader, Wojciech Jaruzelski.
"When I went into a coma there was only tea and vinegar in the shops, meat was rationed and huge petrol queues were everywhere," Mr Grzebski said.
The following year's elections ushered in eastern Europe's first post-communist government.
Poland joined the Nato alliance in 1999 and the European Union in 2004.
"What amazes me today is all these people who walk around with their mobile phones and never stop moaning," said Mr Grzebski.
"I've got nothing to complain about."