http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumatatu, 20 Oktoba 2014

SNP GWAJIMA: IBADA YA JUMAPILI SOMO: SHERIA MBILI ZA ROHONI

SOMO: SHERIA MBILI ZA ROHONI
TAREHE: 19/10/2014
NA MCHUNGAJI KIONGOZI: JOSEPHAT GWAJIMA


 























Kuna ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili. Mtu anapofanikiwa rohoni baadae anafanikiwa mwilini. Inaweza kuwa magonjwa au ukawa na matatizo yakikutokea mwilini jua kuwa yameanzia rohoni. Unapoanza kuomba na kushambulia lazima utambue kuwa unashindana na ulimwengu wa roho.Imeandikwa;
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Waefeso 6:12
Kumbe kabla ya kubarikiwa lazima ubarikiwe rohoni. Tukizungumzia miji ya kiroho, inamaana kwamba ulimwengu wa roho ni sawa na miji unayoiona hapa duniani. Ukiona watu wanajua maneno au mistari ya biblia yote, sio ishara ya kuwa yeye anauwezo wa kuyajua yote na namna ya kushindana. Mungu ni roho, hivyo lazima tumwabudu katika roho. Imeandikwa.
Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; Yohane2:24
Viumbe katika ulimwengu wa roho mfano, Mungu, malaika, mashetani
Viumbe wa kimwili ni kama wanadamu, kuku, simba, miti
Katika ulimwengu wa roho, kuna sheria mbili zinazouongoza. Mambo yote huanzia katika ulimwengu wa roho, hasa katika ndoto. Zipo sheria 2, zinazoongoza ulimwengu wa roho.
1. KUBADILIKA UMBO NA KUVAA UMBO LOLOTE
Ili mashetani ambao ni wachawi ili waweze kwenda kuroga lazima watoke ndani ya miili yao na kuvaa umbo jingine. Kwa kuwa anakuwa rohoni anaweza kuvaa umbo lolote, na kugeuka kuwa kitu chochote. Mfano, paka, mbwa, kunguru. Lakini wachawi wanaposikia hukutambua kuwa ni wachawi wanafurahi sana. Imeandikwa; Marko 16:12
12 Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba.
Yesu aliwatokea wanafunzi wake akiwa na sura nyingine, lakini kwa kuwa alikuwa rohoni, alionekana kuwa na sura nyingine. Yesu anasura nyingine, kama umezoea kumuona daktari leo anasura nyingine, akitaka kukutokea kama mmea natakutokea kama ua la sharoni, au mzee wa siku, lazima utambue kuwa laizima atokee kwa sura nyingine.
Ukiri; leo katika jina la yesu yesu akutokee kwa sura nyingine, kama umezoa yesu ni mponyaji tu leo anasura nyingine, ni mfariji, ni mfalme wa wafalme, ni mwamba wa kale. Leo lazima yesu atokee kwa sura nyingine sawa na tatizo ulilonalo. Amen.
Yesu aliamua kubadili sura lakini wanafunzi wake walijua ni yeye. Kila unapoongezeka kila hatua unaongeza marafi unaongeza maadui pia. Lakini kama ulikuwa umezoea kutembea kama chura tambua kuwa unatakiwa kuruka juu kama tai. Imeandikwa;……………………………. Yohana20;15
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
Nirahisi sana watu kukuamini lakini mtu aliyekuzoea hawezi kukuamini kirahisi, ndiyo maana Yesu alimtokea mama yake kwa sura nyingine kama mtunza bustani, ili aweze kumwamini. Watu wamemzoea yesu wa kuponya magonjwa tu lakini yesu anatokea kwa sura nyingine ili mambo yaweze kutokea na kumwamini.
Hivyo ili uweze kufanya ya rohoni lazima uvae sura nyingine. Imeandikwa; ufunuo 1:9
9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.
10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,
Roho inaweza kuvaa sura yoyote ndiyo maana Yesu alimtokea Yohane katika sura nyingine kwenye kisiwa cha Patmo.. Imeandikwa;
Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari. Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, Mwanzo18; 1-2
Kumbe roho inaweza kugeuka na kuwa kitu chochote, na kufanaya kazi kama wanadamu. Imeandikwa;
Huwafanya malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa moto wa miali. zaburi 104:4
Ukishaona matukio kama hayo unahisi ni upepo kumbe kuna watu ndani ya upepo. Unaweza kuona upepo unakuja ukahisi ni upepo kumbe ni mjomba au bibi yuko ndani ya upepo. Lazima utambue kuwa kuna upepo unaosumbua hali ya maisha yako ndo maana unaona taabu na misukosuko.
Yesu alisema na tuvuke ng’ambo ya pili lakini shetani aliyajua hayo na kutikisa chombo. Tambua hata wewe kwenye maisha yako ukiona umepanga kufanya jambo lolote la maendeleo na mara gafla matatizo yanaanza usikubali pigana maana ni upepo huo umetengenezwa ili usifike unakoenda au usifanye unachotaka kufanya. Imeandikwa;
Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.
12 Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao. Kutoka 7; 11-12
UKIRI
Kuanzia leo kila atakae jigeuza kwa sura yoyote nitamuona kwa Jina la Yesu.
Haimanishi kuwa mashetani wanaouwezo wa kutengeneza chura, au nyoka au fimbo ila tu waliweza kunuizia kitu kikageuka na kutimiza lengo. Malaika anaweza kufanya vile hata mashetani wanaweza kuvaa sura na maumbo ya kitu na kutimiza kusudi. Imeandikwa;
Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.2Wakoritho 11:14
AINA NNE ZA MASHETANI
1. Majoka amabao ni roho ya uovu walioanguka kutoka mbinguni baada ya uasi. Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; Ufunuo 12;7
2. Mizimu. Haya ni mashetani waliotawala ukoo kwa muda mrefu.
3. Miungu. Ni mashetani waliopewa makafara kwa muda mrefu na wakapewa nguvu na kuwa miungu
4. Majini. Hawa nai mashetani wenye asili ya kiarabu.
Imeandikwa;
Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. Ufunuo 16:13
Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza; Ufunuo 18:2
Nguvu kubwa ya mashetani ni ule uwezo wa kutowatambua. Wanapotoka ndani huwa wananuiza na kuvaa maumbo bandia. Wachawi nao huwa wanasikiliza kama umewatambua, wakiona umeona visivyo wanafurahi maana wanajua kuna biashara inaendelea na wamefanikiwa.
Ukiri.
Kuanzia leo lazima kila atakekuja kuniroga nitamuona kwa jina la Yesu.Kila aliyegeuza umbo naamuru nimuone katika umbo lake la siri.
Watu wengine wanajisikia kama wana misumari ndani ya miili yao lakini jambo amabalo hukulijua kama limetengenezwa an kugeuka kuwa kisu ndani ya miili yao. Ukiona nchi inayumbayumba lazima ujue kuna chanzo chake kiko katika ulimwengu wa roho. Ukishinda rohoni unaweza kuua kwa siraha isiyorasmi .
Yawezekana umeumwa sana na hujui namna ya kutatua tatizo ulilonalo.Imeandikwa;
Inawezekana, unajisikia hali mbaya hasa ya kumtukana mume wako, au mke wako lakini kwa akili zako huwezi kusema vile, lakini ukajikuta unasema vile. Kimsingi kuna viumbe wa rohoni wanakaa ndani yako ndo maana wakati mwingine unajikuta umeshatukana.
Inawezekana, unaona uso wako unaweka makeup, lakini sura iko kama babu, jambo usilolijua ni kuwa yuko aliyetumwa na kugeuka na kuwa babu.
MAOMBI
jini, joka, mzimu, aliyegeuka umbo na kuja kwangu, lazima nikuone katika jina la yesu.nina waamuru wapigwe katiak jina la yesu.Mimi ni askari naangusha ngome za balaa, ngome za mikosi, ngome za magonjwa katika jina la Yesu. Mimi nakataa kutawaliwa katika jina la yesu.
Kuanzia sasa roho yoyote iliyogeuka na kuwa balaa, talaka, mikosi, magonjwa, naivunja katika jina la yesu. Kwa jina la yesu kuanzia leo chochote kilichotumwa, nilichikinunua, nakiangamiza katika jin layesu. Kitu chochote, au roho yoyote, iliyondani ya nyumba yangu naivunja, na irudisha ilikotoka katika jina la Yesu.
Kwa jina la yesu,
2. UNAMFUMBA MTU ASIKUTAMBUE.
Katika sheria mbili za rohoni pili ni kukufumba usimtambue, na wewe ukiona unahisi ni vitu hivyo ulivyoviona kwa macho au katika ndoto. Akili ya mtu akifungwa mtu akiona hatambui kama ni wachawi au mashetani. Yawezeka kila ukilala na kuota ndoto ukiamka unaanza kusema uliyoyaota ambayo yako katika sura bandia. Inatakiwa uwafunge ili wasijifiche wakija uwatambuae katika jina la Yesu. Omba maombi haya kwa jina la Yesu. Maana imeandikwa Imeandikwa ;
Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya Yohana 14:13-14
MAOMBI
Katika jina la yesu namteketeza mtu yeyote aliyejigeuza sura ili anitese namfyeka katika jina la yesu.
Kila atakaekuja katika umbo lolote lazima nimjue katika jina la Yesu, ninawafunga wasinitambue kama nimewaona. Kuanzia leo naamka toka usingizi wa kiroho, na akili yangu iwaze kutawala, iwaze biashara katika jina la Yesu . Kuanzia leo naanza kutambua kazi yangu, nianze kuelewa kazi ya kufanya, biashara ya kufanya, katika jina la Yesu.
Nawashambulia mashetani wote katika jina la Yesu, mashetani walioshikiria familia yangu, kazi yangu, ndoa yangu, biashara yangu katika jina la Yesu nawaangamiza katika jina la Yesu. Nawaangamiza maadui wote katika jina la Yes. Natumia mamlaka aliyonipa Yesu nawafyeka wanaozuia kazi yangu nawafyeka wanaozuia ndoa yangu, nawafyeka wanaozuia huduma yangu, katika jina la Yesu. Nawashambulia kwa damu ya mwanakondoo.
Imeandikwa;
Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana. Isaya 54:17
Nawafyeka katika jina la Yesu, mtu yeyote aliyesimama kwenye njia zangu kunizuia nisifanikiwe, kuzuia nisisonge mbele kunizuia nisipate ajira, nafunga uwezo wako wa kujigeuza na kuwa balaa, nakujigeuza kuwa mikosi, kuwa matatizo ,kuwa mtego na balaa, nawashambulia katika jina la Yesu.
Naharibu uwezo wenu katika jina la Yesu, ng’oa madhabahu zenu katika jina la Yesu. Nawatiisha, na kata mamlaka zenu, kaila kiumbe kinachotumia mazira kuharibu maisha yangu nawashambulia katila jina la Yesu. Naaribu uweza wenu wote katika jina la Yesu.
Natangua yote uliyoyapanga katika jina la Yesu. Imeandikwa; yeye uyatangua mashauri ya wadanganyifu na mikono yao isipate kutimiza makusudi yao.
Kila vibarua wa shetani mnaovaa sura bandia nawaangamiza katika jina la Yesu, navunja kila laana ya familia iliyonipata kupitia viumbe wa rohoni mnaojibadilisha sura na kuniroga nawafyeka katika jina la Yesu.
Kila nguvu ya giza inayotawala nailaani katika jina la Yesu, kila balaa zinazotawala nazivunja katika jina la Yesu. Nakiri leo niko huru, kazi yangu iko huru katiaka jina la Yesu. AMEN
Inua mikono juu; na ukiri maneno haya kwa nguvu
Kila jini aliye ndani yangu uliyeingia ili mimi nisiolewe, ili uniletee balaa, imeandikwa lolote mtakalolifunga hapa duniani , litafungwa na mbinguni ewe jini uliyetumwa ofisini kutoka kijijini, nakuapisha dhihirika na ujulikane kwa jina la Yesu. Jini makata, jini wa hasira, jini wa mikosi, kila aliyerogwa kwa kuwekewa dawa kwenye tumbo la uzazi, kwenye maji ya kuoga, kwenye chakula, kwenye kitanda, kwenye nguo, kwenye damu wakati wa siku zangu naamuru moto ndani yangu ukuunguze na unitoke katika jina la Yesu.
-----------------------------------AMEN---------------------------------------------

Jumatatu, 13 Oktoba 2014

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA-

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 12/10/2014

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA

SOMO: HAIKUWA HIVYO TANGU ZAMANI

Utangulizi
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima

 Kanisa leo limefanywa kuwa mahali pa kukutania baada ya uchovu wa wiki nzima. Lakini haikuwa hivyo tangu zamani; kanisa lilianzishwa kama mahali pa kutatua matatizo yaliyoshindikana ndani ya wiki nzima.
“Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha katika tumaini;
Kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote  pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” Warumi 8:19-22

Kumbe kuna viumbe ambavyo vimebebeshwa utumwa wa aina fulani ambavyo vinategemea kuwekwa huru.
Ulimwengu tunaouendea utakuwa ni ulimwengu ambao sio wa kushinda kwa sababu ndugu yako ni mbunge, waziri ama raisi, bali utakuwa ni ulimwengu wa kushinda mambo yote kwa imani. Tunakiendea kizazi ambacho mwenye haki ataishi kwa imani.

“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” Mwanzo1:28
Haya ni mamlaka ambayo Mungu alimpa mwanadamu zamani sana kabla nyumba hazijajengwa, kabla  mavazi hayajaanza kutengenezwa. Kwanza ni kuzaa na kuongezeka iwe mwilini au rohoni. Pili ni kutiisha kila kitu kwenye nchi; mapori, majangwa, milima. Tatu, kutawala kila kitu angani, baharini na nchi kavu. Hivi ndivyo ilivyokuwa tangu mwanzo, asili yetu kama wana wa Mungu ni kutawala sio kutawaliwa. Lakini leo wana wa Mungu wamekuwa watu wakuogopaogopa; sivyo ilivyokuwa. Tuliumbwa kutiisha na kutawala angani, baharini na kwenye nchi.
Mungu ni Mungu wa kusema. Kabla hajatenda huwa anaongea kwanza. Ndio maana biblia nzima imejaa ahadi za Mungu, anasema atatubariki, atatuinua. Hivyo inatupasa  na sisi kuongea na kuikiri asili yetu. Tunatawala kwa mujibu wa sheria ya kitabu cha Mwanzo ibara ya kwanza kifungu cha ishirini na nane. Biblia ni sheria ya Bwana wa Majeshi na sheria hii haiwezi kubadilika kizazi hata kizazi.

Kwa asili ya mwanadamu alitakiwa atawale majini, angani na katika nchi. Shetani alipoona mwanadamu amepewa mamlaka hiyo akamfuata Adamu ili aibe mamlaka hiyo. Kwa kuwa sisi nasi tulikuwa katika viuno vya Adamu wakati anatenda dhambi iliyomgharimu mamlaka yake tumehesabiwa dhambi kutoka kwake..
“Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

Ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tama za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili nay a nia, tukawa kwa tabi yetu watoto wa hasira kama na hao wengine” Waefeso 2:1-3
Ndio maana leo shetani anaitwa mkuu wa anga. Kabla ya Adamu na Eva hawajatenda dhambi walikuwa wanatiisha anga, nchi na bahari. Walipokosea walipoteza mamlaka yao ambayo ilichukuliwa na shetani. Shetani aliichukua anga na kuitawala ndio maana akaitwa mfalme wa anga.
“Nao wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hwakupenda maisha yao hata kufa.
Kwa hiyo shangilieni enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wan chi na bahari! Kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache.” Ufunuo12:11-2
Adamu alikuwa anamiliki anga, bahari na nchi. Shetani alipofanikiwa kumtoa Adam, akafanikiwa kumiliki vyote alivyokuwa anamiliki. Ndio maana sasa kuzimu ina sehemu kuu tatu; angani, baharini na kwenye nchi.
Kama wana wa Mungu ambao tunatakiwa kuishi kwa imani ili kumpendeza Mungu;  kutamka, kusema na kukiri ahadi za Mungu kabla hazijawa bayana katika ulimwengu wa mwili ni sehemu ya maisha yetu. Tamka kwa bidii yaliyomo ndani ya moyo wako kwa maana uweza wa uzima na mauti u ndani ya kinywa chako. Hii ndiyo imani itupasayo kuishi kwayo. Imani ina viwango vinne;

Ø Unachowaza
Awazavyo mtu moyoni mwake ndivyo alivyo. Ni muhimu kujua namna ya kuyatiisha mawazo yako ili yawe sawasawa na namna ambavyo Mungu anawaza kuhusu wewe.

Ø Unachosema
Chochote uwazacho baada ya muda fulani utakikiri kwa kuwa hii ndiyo asili yetu kutoka kwa Mungu; kusema kabla jambo halijatokea.

Ø Unachotenda
  Ukishawaza na kukiri ni lazima uanze kutenda kuelekea kwenye lile jambo ambalo unaloliamini.

Ø Tendo la Imani
Hili ni tendo ambalo unatenda ambalo huwa ni kinyume na hali halisi ya mambo katika ulimwengu wa mwili.
Pasipo Imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Mungu ni Mungu wa makusudi, hivyo lazima ufahamu kusudi lako katika maisha. Maendeleo hayaji kwa kuota utakuwa unatembea ukaokota mamilioni ya fedha halafu ukafanikiwa, mafanikio yoyote huja kwa hatua za kuhifadhi kidogokidogo kile ulicho nacho. Pale ambapo kusudi lisipofahamika matumizi mabaya lazima yatokee.

Hivyo shetani alipomtoa Adamu kwenye utawala akakaa yeye kuwa mtawala wa anga, nchi, bahari na vyote vilivyomo. Kabla Adamu hajatenda dhambi, akiwa bado ni mtawala; sisi tulikuwa ndani ya viuno vyake hivyo tulionja utawala huo. Baada ya shetani kuuchukua utawala kutoka kwetu, ana uwezo wa kuvitiisha viumbe vyote baharini, angani na kwenye nchi. Anayo mamlaka ya kuamuru viumbe kama bacteria, virusi , protozoa kuingia ndani ya miili ya wanadamu na kusababisha magonjwa au hata mauti. Leo dunia ina kila aina ya magonjwa na nyuma ya kila ugonjwa kuna kiumbe. Lakini viumbe hivi vimetiishwa kwa ubatili na yule aibaye ambaye ameiba mamlaka yetu. Haikuwa hivyo tangu zamani.
Mwanzoni Adamu hakuwa na magonjwa kabisa kwasababu alikuwa anatawala anga na viumbe vyake vyote, nchi na viumbe vyake vyote bahari na viumbe vyake vyote. Hivyo viumbe vyote vilikuwa chini ya utiisho wake. Hii ndiyo asili ya mwanzo ya mwanadamu.
Kwa nini leo kila janga kubwa linatokea Afrika? Vita vya kikabila, siasa mbovu, umaskini uliopitiliza, magonjwa ya ajabu; ukimwi unaua sana Afrika, ebola, mafua ya ndege, mafua ya nguruwe, dengue. Ni nini kinatokea? Shetani hawapendi waafrika kwa sababu anajua kutokea kwao ndipo utakapotokea ule uamsho wa siku za mwisho utakaogeuza tawala zote kuwa tawala za mwanakondoo. Imani bado ipo Afrika.
Tangu mwanzo shetani amekuwa akiona dalili za Afrika kuwa jeshi la mwisho la Mungu ndio maana anainua vita juu yake. Wana wa Israeli waliishi Afrika kwa miaka mia nne na thelathini utumwani Misri, miujiza mingi ilitokea Afrika  kule Misri. Haitoshi  alipozaliwa Yesu, malaika alimtokea Yusufu akamwambia amchukue Mariamu mkewe na mtoto Yesu na kuwapeleka katika nchi ya Misri. Wakati wa kubeba msalaba, ilipofika hatua  Yesu hawezi kuubeba tena alitokea Simon mkrene (Krene ni Afrika mahali panapoitwa Libya leo.) akaubeba msalaba mpaka Kalvari. Hii ni kuonyesha kuwa injili ya siku za mwisho itabebwa na waafrika. Ndio maana biblia inasema kutakuwepo na madhabahu katika nchi ya Afrika ( Isaya 19:4) 4 Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, Bwana wa majeshi.
Yesu alivyokuja duniani alikuja kuturudishia utawala wetu ulioibiwa na shetani. Basi kumbe leo shetani anatawala isivyo halali, sisi ndio watawala halali. Tunayo mamlaka ya kuvitiisha viumbe vyote viletavyo magonjwa  kukaa nje ya mipaka ya Tanzania kwa jina la Yesu na vikatii.
Ebola ni mpango wa kuzimu, ni hukumu ya kifo kwa waafrika ili kuipunguza nguvu yetu. Na sisi kama watawala leo tumegundua asili yetu na hila ya yule alaye. Hivyo inatupasa kuchukua hatua kama watawala kutiisha, kumiliki na kutawala.
 
 
Maelfu ya watu wakiomba ndani ya bonde la kukata maneno

MAOMBI.
Ninaamuru kama mtawala wa bakteria, virusi na viumbe vyote wa magonjwa hamna uwezo juu yangu kwa jina la Yesu. Hamna mamlaka juu ya Tanzania. Ninawatiisha viumbe wote wanaoonekana na wasioonekana wasababishao magonjwa kwa jina la Yesu, hamtaingia ndani ya Tanzania kwa jina la Yesu. Kwa mamlaka niliyonayo ninawafunga virusi wote wa mafua ya ndege, virusi wa mafua ya nguruwe, ebola  nje ya Tanzania kwa damu ya Yesu. Kemikali zote, bakteria, protozoa wote ninawatiisha kwa damu ya Yesu Kristo. Kwa mamlaka ya damu ya mwanakondoo, viumbe wote wa magonjwa ninaupiga ule uweza uliowekwa ndani yenu juu ya Tanzania, juu ya Afrika, juu ya maisha yangu, juu ya familia yangu; ninaamuru kuanzia sasa  hamtaingia ndani ya nchi ya Tanzania kwa jina la Yesu.Ninavimiliki na kuvitiisha viumbe vyote vinavyokaa kwenye anga, bahari, na nchi. Mimi ni mtawala wenu, hamna mamlaka ya kunitawala  haikuwa hivyo tangu zamani. Ninawaseta mrudi kuzimu mlikotoka kwa jina la Yesu. Ninaamuru kuanzia sasa hamtanidhuru kwa damu ya Yesu. Viumbe vyote vinavyoonekana na visivyoonekana hamna uwezo wa kunitawala kwa jina la Yesu Kristo. Ninabeba mamlaka kama mtawala, ninawateketeza na uwezo wenu wa kudhuru kwa damu ya mwanakondoo. Nimepewa amri juu ya pepo wachafu na viumbe vyote, ninaangamiza kila nguvu iliyo juu yenu ninyi viumbe wa kishetani na kichawi na waganga wa kienyeji, ninawakausha kwa damu ya Yesu Kristo. Niwaondolea ule uwezo wa kuidhuru Tanzania kwa mamlaka ya damu ya mwanakondoo. Ninaiachilia damu ya mwanakondoo kwenye mipaka yote ya Tanzania,  damu inenayo  mema, ninainyunyizia kwenye mipaka yote ya Taifa la Tanzania na juu ya watu wake wote. Iwalinde dhidi ya magonjwa yote kwa jina la Yesu. Kwa mamlaka ya Jina la Yesu kristo ninatawala viumbe vvyote  vilivyomo baharini,  angani na kwenye nchi kwa damu ya Yesu. Ninatawala uchumi wa nchi, utajiri wa nchi; ninautawala kwa jina la Yesu Kristo. Ninatawala kwa jina la Yesu Kristo, ninatawala na kuvitiisha viumbe vyote vya magonjwa kwa jina la Yesu Kristo. AMEN!
 







 

Jumatano, 16 Julai 2014

UFUFUO NA UZIMA KAWE J'PILI JULAI 13, 2014- SOMO: MASHIMO YA KICHAWI

MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MASHIMO YA KIROHO/KICHAWI
I.                    Utangulizi
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima
Kuna ulimwengu wa aina mbili ; ulimwengu unaoonekana kwa macho na ulimwengu usio onekana kwa macho. Kwanini unaitwa ulimwengu wa roho kwasababu unakaa rohoni na pia kila kinachokaa kule ni roho mfano gari, mtu, mti, nyumba ni roho zinazogeuka kuwa vitu na watu wengi wanaupata kupitia ndoto na ukitaka kwenda kule ni mpaka uwe rohoni na vitu vingi vinaanzia rohoni na uwezo wako wa kushindana kwenye ulimwengu waroho ndio uwezekano wako wa kupokea Baraka za mwili. Wakristo wengi hawatambui taifa linaweza kushikiliwa rohoni, uso wa mtu unaweza kushikiliwa rohoni hata nyumba inaweza kushikiliwa rohoni.
II.                  SOMO.
Waefeso1:33 Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo; 20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 
Waefeso2: 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; 6 Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;   
Waefeso3: 10 ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;     
Waefeso6: 12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 
Akitolewa shimoni
Zamani kwenye agano la kale kulikuwa na  mashimo walikuwa hawana magereza kama ya leo bali yalikuwa ni mashimo marefu sana na ulipokuwa unafanya kosa unatupwa shimoni na kuna aina nyingine ya mashimo ambayo yalikuwa yanawekwa wanyama kama danieli alivyotupiwa kwenye tundu la Simba, na mashimo mengine yalikuwa yana maji na ndio maana ya lile andiko watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa wamefichwa mashimoni wala hapana aokoaye wamekuwa mateka wala hapana  asemaye rudisha. Lakini kwenye agano jipya hakuna mashimo kama hayo bali kuna mashimo ya kiroho ya kichawi ambayo yamejengwa kwenye ulimwengu wa kiroho na wachawi ili kuwaweka watu na ndio maana yesu alipokuja duniani alisema roho wa Bwana yu juu yangu amenitia mafuta niwatangazie wafungwa kufunguliwa kwao.
Ufunuo9: 1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 
2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni. 
Shimo la kuzimu ndio makao makuu ya shetani ni shimo mama lipo kwenye ulimwengu wa rohoni ni refu lisilo onekana linaitwa kuzimu linaitwa shimo la uharibifu, shimo la kifo na hata mashetani walipoasi walitupwa kwenye shimo hilo 2petro2: 2 Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. 
 na hilo shimo ndilo shimo wenye hekima za utawala wanakwenda kuchukua kule au umaarufu wa utawala au nuru ya utawala na sisi tuliookolewa tunapahali petu tunapata ambapo ni Mbinguni juu.  Ndio maana Yesu alisema amelijenga kanisa juu ya mwamba na milango ya kuzimu haita lishinda.
Luka 8: 26 Wakafika pwani ya nchi ya Wagerasi, inayoelekea Galilaya. 
27 Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini. 
28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese. 
29 Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule. Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo, akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo. 
30 Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia. 
31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. 
Miji inaweza kuwa na mashimo ya rohoni na utakaposhughulika na shimo hilo unauteka mji. Mashetani yanamwambia Yesu tunaomba usitupeleke shimoni kwahiyo kila mji kuna mashimo ya kichawi na kuna makao makuu ya utawala wa kishetani matatu nayo ni 1. Shimo la kwanza kubwa la mashetani ni katika nchi “Ufunuo12: 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 
8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. 
9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. ” 2. Katika maji mnyama anapeenme mbili anatokea baharini [pembe ya kwanza ni utawala wa kidini na utawala wa kishetani mwana kondoo maana yake anaonekana mwema] 3. Angani Belzebuli mama wa makahaba anayerutubisha uovu kwa uasherati.
Kuna vishimo vidogovidogo kwenye nchi na unapoona mtu amefariki unasema ameitwa na Bwana kumbe amewekwa mule ndani. Mashimo haya ya kichawi ni kitu gani hasa?. Tulishawahi kujifunza shetani anaweza kuvaa umbo la mtu, malaika walienda kwa Abrahamu wakala wakaongea.  
 Mashetani ni malaika waovu ndio maana kwenye biblia imeaandikwa kuzimu na mauti itawatoa watu wake na ni shimo lisilo na kina na wasiookolewa wote huenda huko.
Mtu ni roho inayokaa ndani ya nyumba inayoitwa mwili  na wanapouzika mwili wanakuwa wameuzika mwili pekee lakini mwenyewe hayupo pale tena.
Luka16: 19 Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. 
20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, 
21 naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. 
22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. 
Mtu anapo kufa anachukuliwa na malaika na anatoka ndani ya mwili anapelekwa kwenye shimo la umilele anasubiri siku ya mwisho atupwe kwenye moto ”na walio kuzimu wanatoka” ila jehanum ndio hawatoki. Sasa unapokuwa umelala unakuwa umechukuliwa na wachawi na kupelekwa shimoni na hata mikono inaweza ikachukuliwa, na ndio maana mtu anapokuwa rohoni analishwa chakula cha kiroho mfano Elia alilishwa mkate na malaika akala akaenda.
Kuna chakula cha rohoni na Neno la Mungu nalo ni chakula cha roho na wachawi nao wanachakula chao Danieli1:7- chakula kimenuiziwa mpaka kimejaa nguvu za rohoni upande wa shetani ndio maana watu wanaota wanakula chakula usiku kimenuiziwa magonjwa, balaa, mikosi, utasa nk. Pia kuna namna ya rohoni uso wako unaondolewa, akili inaondolewa inafichwa kwenye mashimo lakini ukiwa duniani unaanza kuona mara magonjwa ya moyo mara kukataliwa “katika jina la Yesu leo nina amuru ikiwa mimi mwenyewe nimewekwa kwenye shimo ninaamuru leo ninahama kwa jina la Yesu.”
Kwanini wachawi wanamchukua mtu na kumweka kwenye mashimo ni kwasababu unakuta mtu mafanikio yake yamewekwa kwenye uso wake na wachawi wanaweza wakauchukua uso wakaenda kuutumia na mwingine.  wanaweza wakaichukua akili nayo na kuitumia.
Mhubiri9: 11 Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote. 
Kila mtu ana eneo lake la baraka mwingine amewekewa kwenye kinywa wengine kwenye matumbo yao wengine kwenye muonekano na ndio maana wale wenye Baraka zao kwenye uzazi unakuta wanapatwa na shida kwenye kuolewa na hiyo ni kazi ya wachawi wanachukua nyota za biashara na shetani ni mwizi na kazi yake ndio hiyo ya kuiba “sema kwa damu ya Yesu mahala popote walipoweka tumbo la uzazi, macho yangu, kinywa changu, akili yangu au chochoto kwenye mashimo kwa damu ya Yesu mashimo yote yaliyowekwa na familia yangu mashimo yaliyowekwa akili yangu napiga mashimo kwa jina la Yesu naamuru kuanzia sasa akili yangu njoo kwa jina la Yesu.
Ukimwona mtu anamatatizo sana na umekaa naye unazungumza nae kumbe ameshachukuliwa ama amechukuliwa kitu ndani yake uso, mikono, miguu Isaya42:22
Luka4:1-
Hakika Mungu ni mwema
Shetani anamwambia Yesu atampa mali ila masharti yake amsujudu lakini zaburi24 vitu vyote viijazavyo nchi ni mali ya Bwana. Sasa shetani na wachawi wanauwezo wa kuona Baraka na kusudi watu walilowekewa na Mungu ili watumie kufanikiwa na wachawi wanachukua akili za watu na kwenda kumpa mtu mwingine. Mungu anawapa watu vitu mbali mbali na tangu ukiwa mtoto mdogo wanakuja wanakuibia na kuviweka shimoni na kumpa mtu mwingine, unakuta mtu anatabia mbaya lakini anaolewa lakini wewe unatabia nzuri hauolewi kumbe umeibiwa uso wako Mungu ni Mungu wa kurudisha aliwarudisha waisraeli toka utumwani misri na ndiomaana anasema nitakurudishia afya yako, na anaweza kukurudishia afya yako tena, familia yako, bihashara yako. Mungu ni muumbaji na shetan ni mwizi.
Watu wanaofanikiwa wanasiasa, wenye magari hawana Mungu wana mganga wake wa kienyeji. Na kuna watu wanaenda kwa mganga na kumwambia wanataka uongozi na mganga anamwambia njoo kesho na mganga huyu anatoka usiku anakwenda anazunguka anamkuta mtu haombi ana nyota ya uongozi anaichukua nyota hiyo, anatoka anaenda kwa mwingine kuchukua nyota ya kupendwa, anatoka anakwenda kwa mwingine anachukua nyota ya kuongea. Sasa wale waliochukuliwa nyota zao wanaamka hawajui chochote. Unakuta mtu anamatatizo anatamani kufanya biashara lakini hawezi kuisimamia akafanikiwa kumbe wamechukua akili ya bihashara wameficha kwenye mashimo na unamwona mwingine anafanikiwa na hamtumikii Mungu kumbe amepata toka shimoni. sema kwa jina la Yesu kuanzia sasa shimo lolote lenye nyota yangu rudisha kwa jina la yesu.
Makaburini zimelala hazina nyingi ambazo hazijafanyika hapa duniani na hatari kubwa kuliko yote katika maisha ni kufa kabla hujatumia kipaji ulichopewa na Mungu na elimu ni nzuri na ni ya lazima lakini haikuhakikishii mafanikio bali ni taa inayo kusaidia upate kutumia kipaji ulichopewa na Mungu. Kanisani ni center ya walioteswa ni sehemu ya kuwa huru kwa walioonewa. Kuna namna ambayo Mungu anataka uwe na wachawi nao wanaona vile unavyotakiwa kuwa na wanavichukua na unatakiwa uwe mtu wa kupigana kwamaana kushindana kwetu si juu ya damu na nyama maana yake kuna mamlaka za kichawi falme za kichawi tunazotakiwa tupigane nazo ndizo zinazotusumbua. Kuna jambo ambalo wewe umezaliwa ili ulitimize na unapolitimiza jambo hilo na ukafa wewe ni mtu uliyefanikiwa kwa hiyo kuna mtu mwingine amefanikiwa nusu na unaweza usifanikiwe kumbe kuna wanaozuia. Katika jina la yesu hakuna atakaye zuia kila nilichokusudiwa nikifanye kabla sijafa kwa jina la Yesu.
Kwenye kitabu cha yeremia Yeremia anaambiwa na Mungu tangu tumboni nalikujua na kuna watu Mungu amewachagua wawe viongozi na unakuta mama tangu mimba ile imeanza inamatatizo tangu tumboni na unakuta umezaliwa na uunamatatizo lakini kuna jambo lilikuja katikati pale ndilo likaleta maisha uliyo nayo na usishukuru kile ulicho nacho ni mapenzi ya wakala wa kishetani ndio wamekufanya uwe hivyo. Ile akili ya bihashara yako inatumiwa na watu mahali fulani ndio maana shetani anamwambia Yesu nikupe mali lakini hana lolote anataka kuwaibia watu ili aje ampe yesu.
Pengine familia yako imeibiwa au kitu chochote utajuaje umeibiwa? Ndoto unazoziota au unakimbizwa maana yake mashetani yanakufuatilia au uko kwenye kichaka maana yake uko kwenye kichaka cha kishetani unapoota unafanya mapenzi na mtu maana yake unaushirika na mashetani unapoota umevunjika miguu maana yake kuna jambo litatokea upatwe na upofu na kila ndoto unayoota ni jinsi ulivyo rohoni unatakiwa uziharibu ndoto zote mbaya.
Mungu anaongea na watu kupitia ndoto na hakuna ndoto ambayo haina maana na kwenye kitabu cha hatari ya ndoto utakuta unatakiwa ufanye nini unapoota.
Na unatakiwa uchukue hatua na biblia inasema adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake na unakuta mtu ameibiwa nyota yake na mjomba lakini hajui unatakiwa uamue kwa jina la Yesu na utashangaa baada ya wiki moja au mbili utajiri wake unaporomoka wote na anabaki mtupu. Pia mwingine ameibiwa akili na inatokea anashindwa kusoma kwasababu wanajua atafanikiwa kupitia masomo. Pia ndoa nyingine zina baraka wale wanaowaonea wivu wanatengeneza jambo na ndoa yake inavurugika.
Maelfu ya watu wakipiga mashimo ya kichawi
III.                 MAOMBI.
Kwa jina la Yesu nayapiga mashimo ambayo yameweka uso wangu, nayateketeza kwa damu ya yesu mashimo ya kuzimu mashimo ya ukoo mashimo ya familia mashimo ya mashetani mashimo ya wachawi nayapiga kwa jina la yesu nayashambulia mashimo ya ukoo kila shimo lililochimbwa kwa ajili ya kuweka vutu vya ukoo  kila shimo lililohifadhi familia yangu nayapiga kwa jina la yesu kristo, nafanya vita na walinzi wa mashimo nawateketeza kwa moto wa Mungu. Shimo liloshikilia uso wangu nalipiga kwa jina la Yesu, nayashambulia kila mashimo ya kichawi kwa jina la yesu mashimo yote ya rohoni natetekeza kwa jina la yesu nashambulia shimo la kuzimu lililo meza akili zangu kwa jina la Yesu shimo lililoiba uso wangu naliamuru tapika kwa jina la Yesu shimo lililomeza mvuto wangu naamuru kwa jina la Yesu tapika.
Anza kuita chochote ambacho unaona kimeibiwa ita njooooooooooooo kwa jina la Yesu kila kilichofichwa kwenye mashimo njooooooooooooo kwa jina la Yesu, akili iliyofichwa kwenye mashimo njoooooooooooooo kwa jina la Yesu, elimu iliyofichwa njooooooooooooo kwa jina la Yesu, kinywa kilichoibiwa njooooooooooo kwa jina la Yesu, uso uliofichwa shimoni njooooooooooooooo kwa jina la Yesu, Baraka zilizofichwa kwenye mashimo njooooooooooooo kwa jina la Yesu, nafsi za wanadamu njoooooooooooooooooo kwa jina la Yesu kristo……………………………………………
                                         Amen!

Jumamosi, 5 Julai 2014

HALI YA BARABARA IFAKARA - MBINGU ILIVYO NA 'MAHANDAKI'

 1. Hali ya barabara ilivyo mbaya kutoka Ifakara kuelekea Mbingu, magari kuharibika si jambo la kawaida 
 2. Malori yanashindwa safari kutokana na uharibifu wa barabara, hapa linacheua mzigo
3. Barabara zimegeuka bahari kufuatia mvua zilizonyesha hivi karibuni 
4.Gari hili limeshindwa kuhimili ubovu wa barabara, abiria wanateremka ili kulisuma liendelee na safari  
 5. Daraja linalounganisha Ifakara na Mbingu, likiwa limeharibika hata magari kutoruhusiwa kupita kutokana na mvua zilizonyesha na kuharibu miundombinu ya barabara hiyo.
 6.Ni ugumu kupitisha gari dogo katika barabara hiyo, lakini trekta zinatumika kusafirishia abiria
7. Madereva 'wabishi' kama mwenye gari hili aina ya NOAH alilazimisha gari lake kupita katika barabara hiyo iliyoharibika sana

Alhamisi, 3 Julai 2014

MV KILOMBERO II ROHO MKONONI

Kivuko cha mto Kilombero, MV Kilombero II, kimekuwa kikifanya kazi ya kuvusha watu na mali zao, kikiwa hakina msaidizi. Hata hivyo, pamoja na serikali kuwapa zabuni Wachina kujenga daraja la mto huo, kazi yake inaenda kwa kusuasua toka mvua za masika zilizoanza.

Hapa basi la Al Saedy likiingia katika kivuko hicho kuelekea Malinyi, Mahenge

 1. BASI LA AL SAEDY LIKIINGIA KATIKA PANTONI LA MV KILOMBERO II
 2. WASAFIRI WAKIWA NDANI YA MV KILOMBERO 11 PAMOJA NA MAGARI
3. INGAWA KIVUKO NI KIDOGO, BADO KINAVUMILIA MIZIGO MIKUBWA PAMOJA NA WATU

Jumanne, 20 Mei 2014

INGEKUWA BONGO INGEKUAJE? AFUNGWA MIAKA 17 KIMAKOSA

Miaka 17 jela kwa kosa ambalo hakufanya

Victor Nealon
Mwanamume aliyefungwa jela kwa miaka kumi na saba kimakosa ameombwa radhi nchini Uingereza.
Mwanamume huyo alihukumiwa jela baada ya mahakama kumpata na hatia ya kosa la kujaribu kumbaka mwanamke ingawa tume ya kuchunguza kesi za watu waliofungwa jela kimakosa imemuomba radhi.
Victor Nealon, 53, alihukumiwa kwa kosa la kumshambulia mwanamke nje ya ukumbi wa densi mwaka 1996.
Aliomba tume ya kuchunguza kesi za wafungwa waliohukumiwa kimakosa kuchunguza kesi yake ingawa alipuuzwa mara mbili.
Hukumu yake ilifutiliwa mbali mwaka jana.
Tume hiyo sasa imesema ilipaswa kuchunguza kesi yake kwa umaakini ingawa hilo halikufanyika.
Mwenyekiti wa tume hiyo Richard Foster amenukuliwa akisema: "ninajuta sana kwa sababu kuna jambo fulani katika kesi hii ambalo hatukulichunguza vyema, tunamuomba radhi mwathiriwa. ''
'kukosa kuchunguza'
Bwana Nealon, ambaye siku zote alikana madai ya njama ya kumbaka mwanamke , alikamatwa baada ya mwanamke kudai kuwa mwanamume huyo alimdhulumu kimapenzi akiwa anarejea nyumbani kutoka klabuni katika mtaa wa Redditch.
Mtuhumiwa alifungwa jela baada ya mahakama kumpata na hatia na kumhukumu maisha jela.
Alisema kuwa alitaka tume hiyo kuchunguza ushahidi wote uliotolewa katika kesi hiyo.
Mawakili wake hata hivyo ndio waliochunguza ushahidi huo na kupata chembechembe za DNA ambazo sio zake bali za mtu asiyejulikana na kukosoa polisi kwa kuficha ushahidi huo.
Hukumu yake hatimaye ilifutiliwa mbali mwaka 2013.
Alisema: 'Ningekuwa nimeondoka jela miaka kumi au kumi na miwili iliyopita lakini kutokana na kosa la tume kukosa kuchunguza kesi yangu, ilinibidi kuhudumia kifungo kwa kosa ambalo sikufanya.''

bbc

Jumatatu, 19 Mei 2014

MCHUNGAJI GWAJIMA AFUNDISHA SOMO LA MADHABAHU YA UHARIBIFU

Jumapili Mei 18, 2014

Na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima, 18 Mei 2014.





1. 0 Utangulizi

Maandiko ya Msingi: Zaburi 18: 1-50, Waamuzi 6:1-40, 

Kipindi ambacho Taifa la Israel walipokuwa watumwa wa wamidian, watu walikuwa wanaonewa sana na kunyang’anywa mali zao hata mazao yao yalikuwa yakiharibiwa. Hivyo Gidion alikuwa amejificha kwenye mwamba akipepeta ngano ndipo malaika akamwita ewe shujaa Gidion,,lakini Gidion alikataa kuitwa shujaa kwa maaana alikuwa hajiamini. Lakini malaika akamhakikishia kuwa yeye ni shujaa ila ile madhabahu ya Baali aliyokuwa nayo baba yake ndiyo iliyokuwa inamshikilia hata asijitambue kuwa ni shujaa. Hii inatufundisha kuwa kuna madhabahu mahali ambayo inakuzuia wewe usifanikiwe kama Mungu alivyokusudia kwako.

Kwenye madhabahu ile ya nyumbani kwao Gidion kulikuwapo na ashera pia, ashera ni mti uliopandwa kwa ajili ya kusimamia kitu fulani , kwa mfano mti unaweza kupandwa kwa jina la mtu na ule mti ukistawi ndipo mtu Yule anapata matatizo mfano ugonjwa ndiyo maana kuna mtu anakuwa mgonjwa wakati wa masika hii ni kwa sababu ya ule mti unakuwa umenawili kwa mvua. Kuna mtu yuko mahali hapa na watu wasiompenda wamempandia mti eidha wa balaa, magonjwa, umasikini, kukataliwa, kuachwa na kadhalika, lakini leo tunatuma radi na kulipua maashera yote kwa jina la Yesu.

Kwa hiyo Gidion akaambiwa na bwana wewe ni shujaa unatakiwa kwenda kupigana vita ila kwanza bomoa madhabahu iliyo kwenye mji huu inayofanya watu kuwa waoga. Na sisi leo watu wa Ufufuo na Uzima tunaenda kila mahali ilipo madhabahu inayolishikilia Taifa letu na tunaibomoa kwa jina la Yesu. Leo lazima watu wote waliolazwa kwenye madhabahu ya nchi hii watatoka na kuelekea  katika hatima zao na mafanikio yao kwa jina la Yesu.  Gidion baada ya kuibomoa madhabahu ya Baali  watu wa mji walimtafuta ili wamwuue lakini baba yake Gidion (Yoashi) akasema mwacheni baali ajitetee mwenyewe kwa kubomolewa madhabahu yake, kwa hiyo nakutangazia hata wewe leo hakuna dhara hata moja litakalokupata kwa kuzibomoa madhabahu za wachawi .

2.0 MADHABAHU NDANI YA BIBLIA

Mwanzo 8:20, Nuhu alipotoka kwenye safina akamjengea Mungu madhabahu, Hii inaonyesha kuwa kila madhabahu lazima iwe na tukio inaloliwakilisha, kwa mfano kuna madhabahu za utawala, kwa hiyo huwezi kumwondoa mtawala aliye na madhabahu imara mpaka uibomoe ile madhabahu ndipo uguse utawala wake.  Mwanzo 12:7, Ibrahim alipoongea na bwana kwamba nchi ile amepewa ndipo alipojenga madhabahu mahali pale ili isimamie umiliki wake aliopewa kwenye  ile nchi, ndiyo maana hata sasa hakuna mtu anayeweza kuwanyang’anya wa Israel nchi yao ingawa mataifa mengi wamejaribu kuwaondoa lakini wameshindwa. Mwanzo 12:8, 13:14, Utaona watu kwenye biblia walikuwa wakijenga madhabahu mahali ili  isimamie jambo fulani.

Madhabahu ni mahali ambapo wachawi na waganga wa kienyeji  wanakusanyikia , wanapokuwa mahali pale wanatoa kafara za damu na wanakuja na mashitaka ya kuwashitaki watu na wananza kujadili. Kwa hiyo mchawi mmoja anapeleka shitaka la kumshitaki mtu kwa mfano atasema simpendi fulani kwa sababu analinga eti anahela ,au ana watoto wasomi au anapendwa sana na watu hivyo  nataka tumkomeshe. Kwa hiyo wachawi wanasema sawa tutamkomesha na ndipo wanapoanza kumtumia mtu mashetani ya kumharibia maisha yake.  Lakini leo nakutangazia kuwa madhabahu zote zilizotesa maisha yako lazima zibomolewe kwa jina la Yesu.  Ninayo ndoto  na ndoto yangu ni kuwa Falme za dunia zimekuwa Falme za mwanakondoo na hii imeishakuwa kwa maana madhabahu za kichawi zilizozuia injili ya Yesu zitabomolewa zote kwa jina la Yesu.

Mchawi anapenda kumshambulia na kumwuua mtu wa karibu yake kwa mfano kaka, dada, mama, baba nakadhalika. Kwa mfano mtu anataka dada fulani asiolewe kabisa, anapeleka jina lake kwenye madhabahu na kumwaga kafara, kwa hiyo kuanzia pale yule dada hawezi kuolewa kabisa kwa maana madhabahu inakuwa inaongea fulani asiolewe, asiolewe. Mwingine anaweza kuwekwa kwenye madhabahu ya uoga, kwa hiyo hawezi kufanya lolote kwa kuogopa eidha hasara kama ni biashara, ajali kama ni safari, kuachwa kama ni ndoa nakadhalika.

Madhabahu inaweza kuwa kakiwanja fulani ambapo wachawi wanakutanikia na kutoa kafara za damu kwa miungu wao. Mtu anaposhitakiwa na jina lake kutajwa mahali pale ndipo mashetani yanaanza kumwandama na kumharibia mambo yake, kwa hiyo mtu yule hawezi kufanikiwa hata afanyeje mpaka atakapoibomoa ile madhabahu. Madhabahu zinapobomolewa watu wanaachiliwa kwa hiyo wachawi na waganga wa kienyeji wanapata hasara, ndiyo maana Gidion alitafutwa auawe kwa kuibomoa madhabahu ya baali iliyokuwa nyumbani kwa baba yake Yoashi. Leo tutabomoa madhabahu iliyokutesa na kuwalaza  kwenye hiyo madhabahu wale waliokuwa wamekulaza kwa jina la Yesu.

Madhabahu /kiwanja cha wachawi huwezi kukiona kwa macho lakini kipo na wachawi wanakutana pale kila usiku na kuwashitaki watu. Ndiyo maana utaona watu wengi wana matatizo yasiyoisha, kwa mfano kuna mtu amelazwa kwenye madhabahu ya kuachwa kwenye ndoa kwa hiyo utamwona mama ameshaolewa na wanaume watatu nakuachwa na wote bila sababu ya msingi.

Mungu anapotaka kumwinua mtu anaruhusu apitie mambo magumu sana kila upande na asione msaada. Ndipo sasa mtu anapoona hana msaada anakumbuka kumlilia Mungu. Kwa mfano Israel walipokuwa na njaa kali sana mpaka watu wamefikia hatua ya  kula watoto wao, ndipo Mfalme akasema mwambie nabii Elisha kesho saa saba atakatwa kichwa asipotabiri kwa habari ya njaa kwenye taifa la Israel. Baada ya kutishwa ndipo nabii Elisha alitoa unabii kwamba kesho chakula kitapatikana tena kwa bei nafuu sana kuliko hata kabla ya njaa kutokeaa na  kesho yake yakatokea kama vile Elisha alivyosema. Hii inafundisha kuwa mtu unapopata matatizo usianze kulia wala kuwalaumu watu bali wakati huo ni wakatiwa kuutafuta uso wa Mungu ili upate jibu la kukutoa mahali pale.  Usifikiri magumu yanayokupata Mungu amekuacha siyo ni kwamba Mungu anataka uanze kumlilia na kumtafuta yeye kwa moyo wako wote kwa maana aliona umeanza kwenda mbali naye.
Kwa hiyo kuna madhabahu ambayo inaweza kuwa imemshikilia mtu mfano mtu anaweza kuwa amelazwa kwenye madhabahu ya umasikini hata akisoma na kusafiri nchi zote duniani hawezi kufanikiwa. Kwa hiyo ili mtu huyo afanikiwa lazima aibomoea ile madhabahu. Leo kila mtu ataomba kulingana na udhaifu alio nao kwenye maisha yake kwa mfano mtu mwenye hofu ataomba akisema kwa jina la Yesu naibomoa  madhabahu ya hofu iliyonishikilia na kuiharibu kafara waliyoitoa kwenye hiyo madhabahu.   Kwa jina la Yesu leo naamuka na kuondoka kwenye madhabhu walioyonilaza kwa jina la Yesu. Na mtu yeyote aliyepeleka jina langu kwenye madhabahu  hiyo namponda kwa jina la Yesu.

Wakati mwingine madhabahu inaweza kuwa siyo kiwanja bali inakuwa kwenye kitu chochote kile, kwa mfano dada mmoja alikuwa anafanya kazi kwenye kampuni ya tajiri, siku moja yule dada akaingia kwenye ofisi ya boss wake na kuona chupa ndogo lakini ndani ya ile chupa yumo yule dada akiwa hai. Hii inatufundisha kuwa yule dada alikuwa amelazwa kwenye madhabahu ya yule tajiri , kwa hiyo mafanikio aliyonayo yule tajiri ni kupitia nyota ya yule dada. 

3.0 MAMLAKA TULIYOPEWA NA BWANA WETU YESU KRISTO
Mathayo 10:1, kwa hiyo watu wa Mungu tumepewa mamlaka ya kutamka na ikawa na leo tunaenda kuzibomoa madhabahu zote kwa jina la Yesu. Mambo hapa dunia hayatokei yenyewe ila kuna kitu  kinafanywa ili yatokee. Na nguvu ya kufanya mambo yatokee ni uwezo wa mtu wa Rohoni  alionao ndiyo unaleta matokeo mazuri ya mwilini. Kwenye ulimwengu wa Roho unapotamka kwamba navunja madhabahu iliyonishikilia mahali popote itakuwa kama utakanyotamka.

4.0 HITIMISHO
4.1 MAOMBI
Kwa damu ya mwanakondoo naibomoa madhabahu ya wachawi kwa jina la Yesu, mahali popote walipotaja jina langu napaharibu kwa jina la Yesu, Naibomoa hali ya  kuwa kichaa, naibomoa madhabahu ya wendawazimu,naibomoa madhabahu ya mikosi kwa jina la Yesu. Mtu yeyote aliyenilaza kwenye madhabahu yake ya utawala leo naondoka na nakataa kubaki pale kwa jina la Yesu na nyota yangu naimuru ianze kung’aa.

Nakataa watoto wangu , kazi yangu, ukoo wangu kuwekwa kwenye madhabahu ya wachawi kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu ya kifo, umasikini,uoga na mikosi kwa jina la Yesu. Imeandikwa Gidion aliwapeleka watumishi wake kumi wakaibomoa madhabahu ya baali, na sisi watumishi wa Mungu leo tunazibomoa madhabahu zote zilizoshikilia taifa letu na watu  kwa jina la Yesu.  Imeandikwa bomoeni bomoeni hadi msingini, leo nabomoa madhabahu zote, madhabahu ya dhiki, magonjwa, umasikini kwa jina la Yesu. Nabomoa madhabahu ya shaba, udongo, chuma ,mti kwa jina la Yesu. Nakataa kushikiliwa kwa jina la Yesu, mtu yeyote anayenicontrol kupitia madhabahu yoyote leo nakaataa kwa jina la Yesu. Madhabahu ya mabaya iliyoimarishwa naivunja kwa jina la Yesu, mabaya hayatanipata mimi. Naamuru mizimu, majini, majoka anza kuondoka kwa maana madhabahu zenu zimebomolewa kwa jina la Yesu.  Imeandikwa bwana amenifunga mshipi wa vita,  leo nafanya vita na kuziteketeza madhabahu zote na nawachinja makuhani wote wa hizo madhabahu.

Naivunja madhabahu inayoninyima promosheni,inayonizuia nisisafari, inayonizuia nizipate pesa kwa jina la Yesu,.  Na kuhani yeyote aliyenipeleka kwenye hizo madhabahu leo namchinja . Imeandikwa bomoeni bomoeni hadi msingi leo naenda kubomoa madhabahu za njia panda, porini, bahari . Nainyamazisha damu iliyomwagwa kwenye madhabahu za wachawi kwa damu ya Yesu. Ninaamuru kuanzia sasa kila madhabahu inayonena nainyamazisha kwa jina la Yesu. Kila madhabahu iliyojengwa kwenye nchi ya Tanzania ili kukamata akili na nia za watanzania leo nakupasua vipanda vipande kwa jina la Yesu. Naamru na roho zote zilizolazwa kwenye madhabahu zianzae kuamka kwa jina la Yesu. Nakata kamba zote zinazounganisha watu na madhabahu za wachawi kwa jina la Yesu.

Nakata ashera zote zilizopandwa kwa majina ya watu kwa jina la Yesu. Nazilaani ashera zote na kuanzia sasa zianze kukauka kwa jinala Yesu. Nawateka nyara wasimamizi na makuhani wa madhabahu  nawachinja kwa jina la Yesu. Ewe Mungu wa madhabahu nakukamata na kukuteketeza kabisa na enzi yako yote kwa jina la Yesu. Leo naamuru mioyo, nafsi, akili na vyote vilivyoshikiliwa kuachiliwa kwa jina la Yesu. Nauzima moto uliwashwa kwenye madhabahu ya wachawi ili watu wapate magonjwa, kichaa, umasikini , balaa na mikosi kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu iliyojengwa kwenye kichwa, tumbo, kifua  kwa jina la Yesu. Naibomoa madhabahu iliyohai na inayotembea kwa jina la Yesu.

Ufunuo 6:9, kuna roho za watu zinaweza kuwa zimewekwa chini ya madhabahu.  Hata wewe leo unaweza kuwa hapa lakini roho yako imelazwa kwenye madhabahu, sema leo naivunja madhabahu iliyonilaza na toka kwa jina la Yesu. Wachawi wa familia wanaweza kumwuuza mtu na kumpeleka alazwe kwenye madhabahu.  Leo naiteketeza hati ya makubaliano yao ambayo imewekwa kwa jina la Yesu, hati iliyonifanya niuzwe na nibaki madhabahuni leo naichana na kuiteketeza kabisa kwa kwa jina la Yesu.