http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Ijumaa, 28 Juni 2013

16 KUCHUANA MISS REDD'S VYUO VIKUU JULAI 5





WAREMBO 16 kutoka Vyuo Vikuu mbalimbali nchini, wanatarajiwa kushiriki shindano la kumsaka Miss Redd’s Highland, linalotarajiwa kufanyika Julai 5 mwaka huu ukumbi wa SAN SIRO Shekilango Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa shindano hayo, Agnes Mathew alisema washiriki hao wamepatikana baada ya kupata nafasi kutoka vyuo wanavyosoma.
“Tumejipanga vizuri katika shindano hili, kwani washiriki wote wanaendelea kunolewa na mwalimu Bless Ngowi, na kujiweka swa siku hiyo ya Ijumaa pale San-siro Shekilango,” alisema Mathew.
Mratibu huyo alisema mpaka sasa zawadi za washindi bado hazijatangazwa kutokana na kuwasubiri wadhamini waliojitokeza kudhamini shindano hilo la kila mwaka.
Alisema ingawa mwaka jana mshindi wa kwanza alipewa Sh.mil. 2, Sh.mil.1.5 kwa wa pili na wa tatu mil.1, lakini mpaka sasa wadhamini hajawasema lolote kuhusu zawazi za washindi.
Mathew aliwataja baadhi ya washiriki wa shindano hilo la ulimbwende ni Sia Mtui, Feube Urio, Rosemary Alloyce, Nyangeta Kuboja, Avelyne Mathew, Juliet Msacky na Severin Minga.
Katika shindano hilo wasanii wa Bongofleva, Ney wa Mitego na Richie Mavoko watawasindikiza warembo hao.  
Aidha, alisema wadhamini waliojitokeza katika shindano hilo ni pamoja na Redd’s, EATV/Radio, Ngorongoro Conservation, Lake Gas, Coca-Cola, Clouds, Times FM, Grand Villa Hotel, Shamool hotel, Sibuka na Magic fm.
 
Mratibu wa Miss Redd's Highlanders, Agnes Mathew

Ijumaa, 21 Juni 2013

DAVID Beckham azusha vurugu China



KUMETOKEA hamaniko kubwa katika chuo kikuu cha China wakati Balozi anayepeleka ujumbe wa ustaraabu katika soka na kuondokana na rushwa David Beckham alipojitokeza.Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England ambaye yuko China kwa ziara ya siku nne akinadi ustaarabu katika soka, alisababisha msukosuko mkubwa wakati alipojitokeza katika viwanja vya chuo kikuu cha Shanghai Tongji ili kukutana na timu ya chuo hicho.

Wakati akiingia katika eneo la chuo hicho, watu zaidi ya 1000 waliojipanga kumuona waliwazidi nguvu polisi, kuvunja ukuta  hali iliyosababisha hekaheka kubwa aliyoleta majeruhi.