http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumatatu, 27 Mei 2013

AMIN KUTOA MPYA BAADA YA TUZO YA KILI


MSANII wa muziki wa Bongofleva nchini, Amin anatarajiwa kutambulisha rasmi kibao chake kipya kiitwacho ‘Nipoze roho’ baada ya kumalizika kwa tuzo za Kili Juni 11.
Akizungumza na Kwety Mbamba-Bay, Amin anayetamba na kibao ‘Mtima Wangu’ alichomshirikisha Linah, alisema kibao hicho kimeandaliwa katika studio ya Sir round ya jijini Dar es Salaam chini ya prodyuza Ima ze Boy.
“Kwa sasa naangalia kwanza tuzo za Kili, kisha baada ya kumalizika kwake Juni 8, siku tatu za mbele nitatambulisha kibao hiki kipya ili kiweze kuruka hewani,” alisema Amin.
Hata hivyo, Amin alisema kwa sasa yupo katika mchakato wa kuhamasiaha mashabiki wake wampigie kura katika tuzo hizo kupitia kibao alichoimba na Linah kikiwa katika mahadhi ya zouk.