http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumanne, 30 Julai 2013

Juma Pondamali 'Mensah' aibukia BongoFLEVA, atoa 'PESA INATUTESA'

Golikipa mstaafu aliyedakia timu ya taifa Tanzania katika mashindano ya African Cup Of Nations 1980, Juma Pondamali 'Mensah', ambaye kwa sasa ni kocha wa makipa wa timu ya taifa 'Taifa Stars', ameingia rasmi kwenye orodha ya wasanii wa Bongofleva ambao wamewahi kuchezea ligi kuu ya Tanzania.



Unashangaa!!!!! ndio namaanisha Juma Pondamali, ameachia wimbo wake unaoitwa "Pesa Inatutesa" 
Pondamali enzi zake akiwa uwanjani alisifika kwa udakaji wa mbwembwe uwanjani na amewahi kufungiwa kucheza soka mara 5 huku mara 4 mechi alizocheza dhidi ya timu yake, zilivunjika kwa sababu yake.
Msanii huyo amezungumzia pia kama kutakuwa na muendelezo baada ya kuachia ngoma hii, lini alijua kama ana uwezo wa kufanya mziki maana mmmmmhhhhhh!!!!!
Licha ya timu ya taifa, Pondamali amezichezea Pan Afrika na Yanga Sports Cluba zote za Jijini Dar es Salaam.
huu ndio wimbo wake unaoitwa "Pesa inatutesa"

Alhamisi, 25 Julai 2013

MCHA KHAMIS 'VIALLI' HATIHATI KUIKOSA UGANDA CRANES

Na Boniface Wambura, Kampala
KIUNGO mshambuliaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Khamis Mcha ‘Vialli’ anaweza kuikosa mechi dhidi ya Uganda keshokutwa kuwania tiekti ya kucheza Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee dhidi ya Uganda, The Cranes.
 
Kiungo huyo wa Azam FC anaweza kuikosa mechi hiyo itakayopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti.
Wachezaji wengine wote wa Stars wako katika hali nzuri na hata Mcha aliyekuwa, Dadktari wa timu, Mwanandi Mwankemwa amesema anaendelea tayari na wanampa mazoezi mepesi.
Kikosi cha kamili cha Stars ilichoko hapa kinaundwa na makipa Juma Kaseja, Mwadini Ali na Ali Mustafa. Mabeki ni Aggrey Morris, David Luhende, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Nadir Haroub na Vincent Barnabas.
Viungo ni Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Khamis Mcha, Mudhathir Yahya, Salum Abubakar na Simon Msuva. Washambuliaji ni John Boko, Juma Luizio na Mrisho Ngasa.
Stars iliwasili Kampala jana jioni tayari kwa mechi ya kuwania tiketi ya CHAN, Fainali ambazo zitafanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Stars ambayo iliwasili ikitokea jijini Mwanza ilipokuwa imepiga kambi ya siku kumi kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itakwenda Afrika Kusini mwakani imefikia hoteli ya Mt. Zion iliyoko eneo la Kisseka katikati ya Jiji la Kampala.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, Kim Poulsen ameridhishwa na kiwango cha hoteli hiyo, kwani ndiyo ambayo timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) ilifikia Novemba mwaka jana ilipokuja Kampala kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Stars ambayo ilitiwa chachu na Rais Jakaya Kikwete alipokutana nayo Uwanja wa Ndege wa Mwanza wakati ikiondoka kuja Kampala, na kuitakia kila la kheri itafanya mazoezi yake ya mwisho kesho (Julai 26 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kujiandaa kwa mechi ya Jumamosi.
Kocha Kim amesema ingawa mechi hiyo ni ngumu, lakini kikosi chake kimejiandaa kuikabili Uganda kwani wachezaji wako wako vizuri na ari kwa ajili ya mechi iko juu.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari siku ya Jumatatu (Julai 29 mwaka huu). Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
 
IMEWEKWA JULAI 25, 2013 SAA 8:10 MCHANA

Jumanne, 23 Julai 2013

MSANII BONGO MOVIE AVUNJIKA MIGUU AKIEKTI MOVIE KWA KUJIRUSHA GHOROFANI


Na Livingstone Mkoi
Msanii nyota toka kiwanda cha muvi za kibongo nchini Maulidi Mfaume maarufu kwa jina la Gado Balotel sasa amekumbwa na balaa la aina yake baada ya kuvunjika miguu yote miwili pamoja na nyonga kuteguka baada ya kudondoka toka ghorofa ya nne alipokuwa akiigiza filamu ya msanii mwingine aitwae Baga.

Baada Xdeejayz na kituo cha luninga cha DTV kupata taarifa hizo lilipiga hatua ndefu hadi mahala anapojiuguzia msanii huyo ambako ni nyumbani kwa msanii Wilson Fike maeneo ya Home Alone Vijana Kinondoni na kuonana uso kwa uso na msanii huyo aneyeishi na maumivu makali.

Akiongea na mwandishi wetu nyumbani hapo Balotel alisema alikutwa na balaa hiyo wiki mbili zilizopita akiwa Location ndani ya hotel ya Conway iliyopo Magomeni Kagera na wasanii wenzake kama Hemed, Baga, Manaiki Sanga na wengineo wakati wakiigiza.

Balotel aliendelea kusema wakati shughuli za kuigiza ziliendelea na kuna sini moja iliyokuwa inahitajika kuigizwa kwa mfano ikimtaka mtu aigize kama anataka kujirusha kwenye ghorofa lakini asiruke ili kameraman achukue picha achukue shoti hiyo kisha mtu huyo aende chini kisha achukuliwe shoti nyingine ya kujifanya ametua chini.
Msanii huyo aliendelea kusema kuwa nafasi hiyo ilibidi aigize msanii mwenye filamu Baga lakini kutokana na uwoga wa msanii huyo alikuwa akijishauri namna ya kuigiza kuruka ghorofani ndipo Balotel akamtoa pembeni na kumuonesha namna ya kuruka kama Jet Lee huku akimwambie mwenzake hiyo ilikuwa kazi ndogo sana.

Msanii huyo aliendelea kusema kuwa baada ya hapo alijikuta ameruka toka ghorofa ya nne, lakini aliendelea kusema“ Wakati nikiwa bado sijashuka chini njiani nilianza kuhisi harufu ya kifo kwani tayari nimuona Israel mtoa roho akinipungia mkono na hatimaye nilitua chini kwa kufikia miguu,” alisema Ballotel

Hata hivyo, kijana huyo aliongeza kusema kuwa mara baada ya kutua chini alihisi moto unawaka miguuni mwake huku harufu ya damu ikimtoka puani na mdomoni na baada ya kujiangalia aliona visigino vyake vikiwa vimepasuka vyote huku tumboni kukiwa na maumivu makali sana kumbe wakati huo nyonga ilikuwa imeachia huku miguu yake ikiwa imesogea tumboni.

Gado alisema baada ya tukio hilo wasanii wenzake walimchukua na kukmimbiza Hospital ya Mwananyamala mbapo dakika chache baadae walimkimbiza Muhimbili kwa matibabu zaidi. Msanii huyo ambaye ametamba sana kwenye filamu kama Going Bongo, Msitu wa Hifadhi,Tumbo Joto na Escap ambayo alikuwa akiigiza siku ya tukio lililomkuta.
Aidha, msanii huyo aliendelea kusema kwa sasa anaishi akiwa na mateso makali huku wasanii wenzake wakishindwa kumpa ushirikiana.

“Hapa nilipo nalelewa na Fike Wilsoni ambaye ananibeba kwenda chooni na kunirudisha kwa kweli hali yangu sio nzuri nahitaji msaada wa wasanii wenzengu, wako wanaokuja kunirushia chochote kama Kalapina,Young Killer na madaktari wanasema huenda wakanishauri kwenda India ili wakazirekebishe nyonga zangu” Alisema Gado na kuongeza kuwa anawaomba wasanii wenzake wasamaria wema kumsaidia kwani hali yake ni mbaya na huenda kwa mujibu wa madaktari wake akahitajika kupelekwa India ili kukinusuru kiuno chake la sivyo hatozaa tena kwa vile nyonga vimeshafyatuka.