http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumatano, 10 Julai 2013

Juma Nature, Mkoloni, pacha Ant-Virus watoa 'Alisema Mwalimu'

1. Nature2. Mkoloni

WASANII wa muziki wa BONGOFLEVA nchini, Juma Nature, Mkoloni na mapacha wa Ant-virus kwa pamoja wameibuka na kibao kipya kiitwacho ‘Alisema Mwalimu’ kilichotokana na milipuko ya mabomu ya mara kwa mara nchini.
Nature amesema kibao hicho kimerekodiwa Halisi Records na kuwashirikisha wasanii hao walioungana kwa pamoja kuzungumzia wosia wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuhusu taifa la Tanzania.
“Tumeshirikiana kwa pamoja katika kibao hicho ili kuelezea hisia zetu na meseji aliyoiacha Baba wa Taifa kuhusiana na amani ya nchi yetu…hivyo kibao hiki cha ‘Alisema Mwalimu’ kitafikisha ujumbe,” alisema Nature ambaye kwa sasa ni prodyuza.
Aidha, alisema katika kuelekea mfungo wa Ramadhani, kundi lake la Wanaume Halisi halitakuwa likifanya shoo yoyote hadi hapo siku 30 za kufunga zitakapokamilika.