http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumanne, 31 Desemba 2013

UKUMBI WA KISASA 'BAY VIEW' ULIOPO KATIKA MJI WA MBAMBA BAY WILAYA YA NYASA SIKU ULIPOZINDULIWA MKESHA WA KRISMASI 2013

 1. Ukumbi wa BAY VIEW ukionekana kwa nje
 2.Watoto wakisubiri kuingia BAY VIEW
 3. Mlango mkuu wa kuingilia BAY VIEW
 4. Watoto wakiserebuka ukumbini
 5.DJ Kiberiti Junior akifanya mambo
 6.DJ Kibiriti Junior akidondosha moja moja kwa watoto
 7. Watoto walisendelea kupata kuburudani ya Disko Toto ndani ya BAY VIEW
 8. Meneja wa BAY VIEW Hussein
 9.Watoto nao hawakuacha tabasamu nyumbani
10. Watoto walifurahi zaidi
11.BAY VIEW ikionekana kwa nje

Jumanne, 10 Desemba 2013

MAHUBIRI YA JUMAPILI TOKA KANISA LA UFUFUO NA UZIMA KAWE DSM. SOMO:KUWAFYEKA WATUNZA KUMBUKUMBU



Senior pastor Josephat Gwajima
Utangulizi
Kwenye biblia shetani anaitwa mshitaki wa ndugu. Ufunuo 12:10. "Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.".1Petro 1:8
Mahakama nyingi hazifanyi kazi usiku, lakini mahakama ya mshitaki huyu inafanya kazi saa ishirini na nne, .
Mtu hawezi kufungwa mpaka kuwepo na mashitaka, kwa kawaida mtu anapokamatwa na polisi huwekwa mahabusu, halafu polisi huandaa hati ya mashitaka na mtu hupelekwa mahakamani, kwenye mahakama za juu hati ya mashitaka huandaliwa na mkurugenzi wa mashtaka (DPP).  Na hati zinaandaliwa ili mtu afungwe.
Sasa shetani ndiye mkurugenzi(wa rohoni) wa mashtaka.  Zaburi 109:6, Uweke mtu mkorofi juu yake, Mshitaki asimame mkono wake wa kuume’.  kuna washitaki wakorofi. 
Mashitaka dhidi ya Yesu, pilato alikuwa mgumu kushughulikia  swala hilo sababu hakukuwa na hati ya mashtaka. Matendo 25:27 "Kwa maana naona ni neno lisilo maana kumpeleka mfungwa, bila kuonyesha mashitaka yale aliyoshitakiwa".  
Mtu hawezi kufungwa isipokuwa ameshtakiwa. 
Hakuna gereza analoweza kuingia mtu bila mashitaka.  Polisi ni watekelezaji wa sheria, ukifanya kosa unakamatwa, na ofisi wa DPP inaandaa mashtaka, hivyo hata katika ulimwengu wa roho kuna idara kabisa ya kuandaa mashtaka na mtu hawezi kufungwa na magonjwa,umasikini au shida ya namna yoyote mpaka yawepo mashitaka.
Kisa cha kweli
Mwaka juzi shetani alinitokea na kuniambia kwa kuwa tumeshampiga sana, basi sasa kila mtu achukue nyaraka zake twende mahakamani, mim nikawaza mahakama gani anayozungumzia..? kama ni ya Mungu, Mungu ni baba yangu na anakaa ndani yangu.. pia nikagundua unapoenda na shetani mahakamani lazima uwe makini la sivyo utaweza kuishia jela.
  
Kolosai 2:3-14 "akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;  akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;"
Yesu alipokuwa msalabani pia alifuta hati za mashtaka kulingana na hukumu zake Yesu!
 Iko hivi mfano Mungu amesema mshahara wa dhambi ni mauti, sasa wewe unapotenda dhambi mashetani wanaandika na wanaangalia kwenye sheria za Mungu wako wanaangalia mfano umezini, wanaenda mbele za Mungu na kushitaki kuwa huyu amezini na wewe umesema mshahara wa dhambi ni mauti tunaomba tukaitimize hiyo sheria.
Mungu akikaa kimya wanajua ndo imekubalika, mashambulizi yanaanza.  Mungu aliwahi kunionyesha jinsi mashetani yanavyoshtaki…
Shetani ni mkurugenzi wa mashtaka, mapepo ni watekelezaji wa hayo mashtaka.  Biblia inasema Mungu si mwepesi wa hasira, ila pia hawezi kumwacha mtenda dhambi bila adhabu.  
Yesu alipokuwa duniani aliletewa mwanamke aliyekuwa akizini, na wakamwambia kwa taratibu za kiyahudi huyu mtu anatakiwa apondwe mawe hadi kifo.  Yesu hakuwakatalia ila akawaambia ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumponda mawe, wale mafarisayo wakaondoka mmoja mmoja ndipo Yesu akamwambia Yule mwanamke washtaki wako wako wapi? Kama wameondoka basi na mimi siwezi kukushitaki enenda kwa amani.
Kwa hiyo kilichomponya yule mwanamke ni wale washitaki wake kuondoka.  Washitaki ndio chanzo cha tatizo.  Hivyo hata wewe kwa jinsi unavyokuwa na washitaki wengi ndivyo kwa jinsi hiyo hiyo matatizo makubwa yatakavyokupata, kwasababu wana tabia ya kuweka kumbukumbu
Kuna idara maalum ya kumbukumbu, ambayo wanapotaka kukushughulikia wanayachukua na kuyapeleka kwa Mungu!  Yaani hiyo ni idara ambayo inasimamiwa na mapepo maalum wanatunza toka makosa ya mababu zako.  Hakuna gereza bila mashitaka.
‘Kwa jina la Yesu leo napiga watunza kumbukumbu wote, kwa jina la Yesu’
Kuna wengine wamefungwa toka tumboni kutokana na madhambi ya mababu na mabibi zao!  Mfano bibi  alikuwa mchawi, wanachofanya mapepo wanakwenda mbele za Bwana na kutoa mashtaka kuhusu familia yako.  Wanamwambia kwa kuwa bibi yake alikuwa mchawi na aliwazuia wengi kuolewa na huyu haturuhusu kumzuia kuolewa, Mungu akinyamaza tayari ndo tiketi ya wao kukuvuruga.  Mungu hawezi kukuadhibu ila mashetani ndo hutunza kumbukumbu na kwenda kukushtaki mbele za Bwana kwa kutumia sheria za Mungu.  Ndio mana inatokea mtu yanampata mabaya wakati hakutenda kosa lolote
"Kwa jina la Yesu, nashambulia watunza kumbukumbu wote wanaotunza kumbukumbu za familia yangu na ukoo wangu"

Ijumaa, 22 Novemba 2013

NGUGI WA THIONG'O AWAUMBUA VIONGOZI WA KIAFRIKA KUTOENZI LUGHA ZAO

Mwanazuoni na Mwanafasihi mahiri Duniani, Ngugi wa Thiong'o amewaumbua wasomi na viongozi wa Afrika kwa kukimbilia lugha za kigeni na kutoenzi zile za Kiafrika.
Ngugi ametoa Muhadhara leo katika CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM).

 1. Prof. Ngugi wa Thiong'o akitoa mhadhara katika ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo.
 2. Ngugi wa Thiong'o
 3. Ngugi akiendelea kutoa mhadhara kwa lugha ya Kiswahili
 4. Ngugi akifurahia jambo
 5.Baadhi ya washiriki katika mhadhara uliotolewa na mwanazuoni Ngungi wa Thiong'o
 6. Watu mbalimbali wakiwemo Maprofesa na wahadhili mbalimbali wakimfuatilia kwa makini Ngugi
 7. Hawa nao walikuwepo
  8. Juu na chini ya ukumbi wa Nkrumah walifurika watu kumsikiliza mwanazuoni na mwanafasihi Ngugi wa Thiong'o

Jumatatu, 18 Novemba 2013

IBADA KUTOKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA KAWE DSM NA MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA

IBADA KUTOKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA KAWE,DSM NA MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA

Mch.Kiongozi Josephat Gwajima
SOMO: VITA NA WALIOKUFA KATIKA DHAMBI
Jumapili Tarehe 17.11.2013

Na Mch. Josephat Gwajima

Nimeamua kuliita hili somo vita sababu tunakwenda kupigana vita moja kwa moja na majeshi ya wafu waliokufa katika dhambini

1 Samwel 28:6-20

“…Ukanipandishie yeye nitakaye mtaja kwako…” tunaoana hapa mfalme anakwenda kwa mganga wa kienyeji anaomba apandishiwe mtu aliekufa miaka mingi, Hapa tunaona kumbe mtu aliekufa anaweza kupandishwa na waganga wa kienyeji kutoka kuzimu na akapanda/akazuka.  
1 Samwel 28:11 “…Nipandishie Samwel...” hapa tunaona Samwel alikuwa amekufa lakini mfalme sauli anamwambia mganga wa kienyeji nipandishie Samweli. 
1 Samwel 28:15 “…Ndipo Samwel akapanda na akamwambia mbona umenitaabisha mimi hata kunipandisha juu...”  Kumbe mtu aliekufa anaweza akapandishwa na akazuka kikweli kweli (Samweli akazuka juu),  
1 Samwel 28:19 “….Tena pamoja na wewe Bwana atawatia Israel mikononi mwa Wafilisti; hata na kesho wewe na wanao mtakuwepo pamoja nami…” Haya ni maelezo anayoyatoa Samweli baada ya kuzuka juu. Akatoa maelezo kwamba baada ya siku tatu utakufa wewe na wanao na mtakuwa mahali hapa name, yaani na nyie mtapandishwa kama mlivonipandisha mimi.

Ukisoma theolojia kuna ubishani mwingi unaendelea, wanatheolojia wengi wanasema sababu Samwel alikuwa mtu wa Mungu, sasa ilikuaje mpaka mganga wa kienyeji akaweza kumpandisha, hivyo husema huyu hakuwa Samweli bali ni pepo (Samweli feki). Lakini mimi nataka nikuambie kuwa huyo alikuwa ni Samweli mwenyewe ndio maana aliweza kumpa maelezo mengi sana, ikiwemo kwamba wewe umemuacha Bwana, na umeamua kunitaabisha kunipandisha juu, hivyo baada ya siku tatu wewe na familia yako mtakufa.

Mfalme Sauli alipoona hajibiwi kwa maono wala kwa ndoto, ndio maana akaamua aende kwa mganga wa kienyeji, ndio maana mimi huwa na kwambia kila kiongozi ambaye hajaokoka anamganga wake wa kienyeji, Mwanadamu kwa asili huwezi ukawa mtupu, ni lazima uwe umeungamanika na madhabahu ya mwanakondoo ama madhabahu ya lusifa. Mimi mwenyewe unavyoniona hapa kuna mamlaka nyuma yangu nimeungamanishwa nayo. Usifikiri leo Ufufuo na Uzima tupo hivi, ukadhania tumeibuka buka tu, hapana kuna vita huko nyuma tumepigana.


Sauli amekwenda kwa mganga wa kienyeji akaomba apandishiwe Samweli ili amuulize limpasalo kutenda. Sauli alijificha ili asijulikana na mganga wa kienyeji kama ni mfalme, maana wafalme walikuwa hawaruhusiwi kwenda kwa waganga wa kienyeji. Baada ya mganga wa kienyeji kuanza kumpandisha Samweli alipiga kelele, akamwambia mbona umenidanganya, (mganga wa kienyeji viliumana na samweli alivokuwa anazuka), Sauli akauliza kwanai anayezuka ni nani akamwambia akasema ni mzee anamavazi meupe anazuka katika nchi. Hapo usifikiri kiliwekwa kikopo cha maji, Sauli akamuona Samweli kwenye maji hapana, Samweli alipanda akaanza kuongea ndani ya mganga wa kienyeji. Inanifurahisha hiimaana mganga wa kienyeji badala ya kupandisha vibwengo akapandisha Samweli, na Samweli akatoa maelekezo.

Mchungaji Kiongozi,Josephat Gwajima, akihubiri ndani ya nyumba ya ufufuo na uzima, Kawe, Dar es Salaam

Watu wakifa wanakwenda wapi?

Kabla Yesu hajafa msalabani kuna sehemu ilikuwa inaitwa shiol hili neno ndio hilo limetafsiriwa na biblia linaitwa kuzimu, yaani ulimwengu wa wafu, ama eneo wanalokaa wafu. Waliokufa katika dhambi ama waliokufa katika haki. Shiol ilikuwa imegawanyika sehemu mbili shiol ya watu waliokufa katika haki na shiol ya watu waliokufa katika dhambi, na hii ilikuwa kabla Yesu hajafa msalabani.  
Mwanzo 37:35 “…Nitamshukia mwanangu hata kuzimu nikiwa nasikitika…” Yaani hapa Yakobo anamaanisha akifa atamshukia mwanae Yusufu huko kuzimu, hii ilikuwa ni kuzimu ya waliokufa katika haki.  
Torati 32:22 “…Moto umewashwa kwa hasira yangu unateketea hata chini ya kuzimu…” Hii ni kuzimbu ya waliokufa katika dhambi.

“Kusimu upande wa wenye haki, na kuzimu upande wa waliokufa dhambini Kabla ya Yesu Kristohajafa msalabani”

1 Samweli 2:6 “…Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu…” Zaburi 6:5 “…Maana mautini hapana kumbukumbu lako; katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?...” Zaburi 16:10 “…Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu…” Yuda 1:6 “...Amewaweka vifungo vya milele chini ya giza…” kuzimu kwa lugha ingine ni chini ya giza kwenye vifungo vya milele.

Yesu alipokufa akashuka kuzimu ya waliokufa katika dhambi akamnyang’anya yule joka ufunguo wa kuzimu na mauti, halafu akaeleke upande wakuzimu ya Ibrahimu (kuzimu ya walikufa katika haki) akawaambia yule uzao wa mwanamke ndio mimi, akawahubiria manabii wote huko kuzimu, na kuwaambia nimekuja kuwahamisha twende juu mbinguni, huku sio mahala penu. Yale makaburi kufunguka ilikuwa ni ishara ya uhamisho wa watu wote waliokufa katika haki kutoka kuzimu ya chini na kwenda mbinguni (paradiso) kule Yesu anakaa. Yesu akawaambia sasa tunahama huku tunaenda paradiso. Kwa hiyo baada ya hapo kuzimu ikawa ni mahali pa wafu waliokufa kwatika dhambi na paradiso (mbinguni) ikawa ni makao ya waliokufa katika haki huko wakimuimbia Mungu,na kufurahi.

Sasa kama vile Samweli alivyopandishwa kutoka kuzimu, kaganga kamama kakampandisha Samweli juu, hivyo ndivyo ambavyo leo mtu aliekufa katika dhambi inawezekana akaitwa na waganga wa kienyeji na akaja, wakamtumia kuharibu ukoo kama wawezavyo, Samweli alipanda lakini mganga alishindwa kumpa maelekezo sababu alikuwa mtakatifu akiwa duniani, lakini mababu na mabibi waliokufa katika dhambi wakipandishwa wanaamrishwa wafanye kile mganga anataka.


Kama tulivyoona aliekufa katika haki akaenda mbinguni, humuimbia Mungu na kufurahi huko mbinguni, na wale waliokufa katika dhambi hushuka kuzimu (kifungoni) na kutumika kwa kazi za kuzimu. Na ndio maana leo nasema lazima tupigane nao vita.

Unapokata roho huwa kuna malaika maalumu wanaochukua roho yako, kama ulikuwa unatenda dhambi malaika wa giza wanabeba roho yako wanashusha mpaka kuzimu(gereza la milele), na kama ulikuwa unatenda haki, malaika kutoka mbinguni wanabeba roho yako na kuipeleka mbinguni (pradiso), Ufunuo 20:13. “…Kuzimu ikawatoa watu waliokuwa ndani yake…” Kuzimu ni makao makuu ya shetani, na ziwa la moto ni sehemu ya hukumu ya wale waliokufa katika dhambi, ukishafika hapo unakuwa mfungwa, na unaanza kumtumikia shetani. Babu yako yule aliekufa katika dhambi yupo kuzimu hajakaa tu kule, yupo anapiga mzigo huko, ndio maana utasikia watu tunaowarudisha msukule hapa, ama watu waliokuwa wamekufa wakifufuka hapa kwetu utasikia kazi yangu ilikuwa ni kwenda kwenda kuua watoto wadogo mahosipitali wengine utasikia nilikuwa nasababisha ajali barabarani, hizo ndizo kazi za wafu huko kuzimu.

Mtu anajiuliza hivi watu wanawezaje kumtupia mtu mapepo hata 1000, unauliza huyu ana akiba ya mapepo kiasi gani, kumbe mengine sio mapepo bali ni watu waliokufa wanatumikishwa na shetani, wapo kuzimu lakini wanatumwa kuja duniani, na huwa wanatumwa kwenye koo zao kufanya uharibifu sababu wao wanazijua hizo koo zao vizuri, ni rahisi kushambulia kwa mafanikio makubwa. Kwanza wanafahamu lugha ya ukoo wenu, wanamfahamu baba wa ukoo, wanafahamu madhaifu yenu yote, ndio maana vita yako huwa inakuwa kali kweli. Shetani huwa anawatuma anawaambiakama vile wewe ulivyokuja huku katuletee shangazi yako, ndio maana utasikia watu wanalalamika bibi yangu alikufa kwa kansa na mama yangu nae kwa kansa na mimi nina kansa sasa hivi, huu ni ugonjwa wa ukoo! Hakuna ugonjwa wa ukoo ni wafu wanatenda kazi katika ukoo.

Makundi yanayoshambuliwa sana na majeshi ya wafu

1.   Wale wanaochukua majina ya ndugu wa ukoo ambao hawajaokoka (majina ya mabibi, mababu, shangazi).

Tuangalie sana majina tunayowapa watoto, utasikia mtu anamwita mtoto dragon, astrorogy, au momony angalia utalia, usimpe majina ya ndugu wa ukoo waliokufa watoto wako kama hujui maana yake, chagua majina yanayompa utukufu Mungu, Glory, Ruth, Grace….

Kwanini agano jipya linaanza na kutaja ukoo wa Yesu?

Hii walitaka kutuonesha kwamba ukoo wa Yesu hauna mganga wa kienyeji, wala msoma nyota, wala darweshi, wate walikuwa watu wa haki.

2.    Wale wanaopenda/wanaoendekeza  mila za familia

Utasikia desturi ya ukoo wetu ndugu yeyote anaekufa wote tutanyolewa vipara, mtoto akizaliwa lazima kitovu apewe shangazi, lazima tukajengee makaburi ya babu. Ukiwa unashiriki hizi taratibu lazima majeshi ya wafu yatakupata tu.

3.    Wale wanaopenda makabila kuliko kumpenda Mungu

Namna ya kuomba

Kwa jina la Yesu ninajitenga kabisa, na watu waliokufa kwenye dhambi. Mimi ni wa ukoo wa Yesu, ninajitenga na nyie kwa jina la Yesu. Jina lolote la mtu alielala katika dhambi, ninajitenga nalo kwa jina la Yesu

Jitenge na umasikini wa ukoo, umasikini wa bibi, umasikini wa babu, umasikini wa shangazi, jitenge na ukoo wako kwa damu ya Yesu, najitenga kutoka babu nababu na babu, nawaamuru muachie mali zangu, achia afya yangu, kata kamba zote za ukoo, kamba za familia kwa jina la Yesu.

NGOMA MPYA: DARASSA FT. MCHIZI MOX & SHILOLE - MIKONO JUU

NGOMA MPYA: DARASSA FT. MCHIZI MOX & SHILOLE - MIKONO JUU

Hii ni moja kati ya ngoma ambazo zipo ndani ya MixTape mpya inayoitwa Dream Big ya rapper Darassa ambayo ameachia Weekend hii.
Ambapo ngoma hii ya Mikono Juu ambayo amemshirikisha msanii Mchizi Mox pamoja na mwanadada Shilole ndio ngoma ya kwanza kabisa kati ya ngoma 19 ambazo zilizopo ndani MixTape hiyo.

Jumanne, 12 Novemba 2013

Kizungumkuti cha amani kati ya M23 na DRC

 12 Novemba, 2013 - Saa 05:15 GMT

DRC ilisusuia shughuli ya kutia saini mkataba wa amani kutokana na maandiko yake
Shughuli ya kutia saini mkataba wa amani kati ya waasi wa M23 na serikali na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,iliyokukuwa imepangwa kufanyika Jumatatu , iligonga mwamba.
Hii ni kutokana na serikali ya Congo kusema kuwa mkataba huo uangaliwe upya na hivyo kulazimisha shughuli hiyo kuahirishwa.
Mpatanishi wa pande hizo mbili Ofuono Opondo wa Uganda, alisema kuwa pande hizo hazikuwa tayari kuonana ana kwa ana baada ya DRC kusema kuwa M23 watie saini mkataba katika chumba tofauti na kisha wapewe wao kuusaini.
Hata hivyo mpatanishi alisema haiwezekeni kwa hilo kufanyika kwa sababu pande zinazozozana lazima zikae katika chumba kimoja kwa ajili ya kufanikisha juhudi za upatanishi.
Kundi la waasi la M23 lilisitisha uasi wao baada ya kupata kipigo kutoka kwa wanajeshi wa DRC wakisaidiwa na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa waliowafurusha kutoka maficho yao ya milimani katika mpaka wa Rwanda na Uganda.
Mkataba huo ulistahili kutiwa saini mjini Kampala Uganda, ingawa shughuli yenyewe ilicheleweshwa bila ya kujua itafanyika lini.
Mwandishi wa BBC mjini Kampala, Ali Mutasa anasema kuwa mpatanishi mkuu Ofwono Opondo alisema mkataba hautatiwa saini na kwamba haijulikani ni lini makubaliano hayo yatasainiwa. Alisema Upande wa M23 uko tayari kwa shughuli hiyo na kuwa kizungumkuti kimetokana upande wa DRC.
Serikali ya DRC kupitia kwa msemaji wake,Lambert Mende ilisema kuwa Kinshasa iko tayari kutia saini makubaliano hayo, lakini sio mkataba unaosema ni makubaliano ya amani kwa sababu ni kama kundi hilo bado lipo.
Duru zinasema kuwa Rais Yoweri Museveni pamoja na wanadiplomasia wa nchi za Magharibi, walisburi mkataba kutiwa saini lakini wajumbe wa DRC hawakuingia katika chumba cha hafla hiyo ya kutia saini.

Ijumaa, 8 Novemba 2013

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA WA KANISA LA UFUFUO NA UZIMA AKABIDHIWA TUZO NA MAASKOFU


Umoja wa wachungaji wa makanisa ya Kipentekoste mkoani Kilimanjaro (PPK)wamempa tuzo ya heshima kanisa la Ufufuo na Uzima kwa mafanikio yao katika kumtangaza Kristo. Tuzo hiyo imekabidhiwa tarehe 30 mwezi uliopita ikiwa ni siku tatu toka kumalizika kwa mkutano mkubwa wa injili ulioandaliwa na mchungaji Gwajima chini ya kanisa lake katika viwanja vya mashujaa mjini Moshi.

Tuzo hiyo ya heshima yenye picha ya mlima Kilimanjaro ilitolewa na mchungaji kiongozi wa umoja huo Samweli Yohana katika ukumbi wa hosteli za Umoja kanisa la Kilutheri Moshi mjini. Mkutano wa wiki moja uliofanyika viwanja vya mashujaa mjini moshi ulivunja rekudi ya idadi ya wahudhuriaji na watu kutoka dini tofauti.

Picha zifuatazo ni matukio ya kukabidhiwa Tuzo hiyo





Alhamisi, 7 Novemba 2013

AKIMBIA MBWA MWITU ALIWA NA MAMBA

NGIRI AKIAMINI AMEWASEVU MBWA MWITU WALIOMZUNGUKA, LAKINI NYUMA YAKE MAMBA AKIFURAHIA KITOWEO (ANGALIA MSHALE). NGIRI HUYO HAKUWEZA KUSALIMIKA KWANI ALIISHIA MDOMONI MWA MAMBA

FOLENI KUBWA YA WAKAZI WA GONGO LAMBOTO WAKIJIANDIKISHA VITAMBULISHO VYA TAIFA

WAKAZI WA GONGO LA MBOTO WAKIWA KATIKA FOLENI YA NDEFU MAENEO YA KITUO KIPYA WAKISUBIRI KUJIANDIKISHA VITMABULISHO VYA TAIFA

Azam FC ya Tanzania yamtimua kocha Stewart

Stewart Hall kocha wa Azam FC

Huku ligi kuu soka Tanzania Bara ikiwa imekamilisha mzunguko wake wa kwanza hii leo,timu ya Azam FC ya Dar es Salaam imetangaza kusitisha mkataba na kocha wake mkuu Stewart Hall wa Uingereza kwa kile kilichoelezwa kama makubaliano ya pamoja.
Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa klabu hiyo jijini Dar es Salaam, hii itakuwa ni mara ya pili kwa kocha huyo kuachana na klabu ya Azam na ameafikiana na uongozi wa klabu hiyo baada ya kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ambapo timu ya Azam sasa inashika nafasi ya Pili baada ya kwenda sare ya mabao 3-3 na timu ya Mbeya City ambapo zote sasa zina Pointi 27. Bingwa mtetezi timu ya Yanga inaongoza ligi hiyo kwa sasa ikiwa na pointi 28 baada ya kuinyuka Oljoro JKT mabao 3-0 katika mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo, maaruf kama Vodacom Premier League.
Klabu ya Azam FC inayoinukia kwa ubora wa miundo mbinu huku ikiendeshwa kisasa kwa mipango inayoeleweka kinyume na klabu nyingi nchini Tanzania imekuwa ikifanya vema chini ya mwalimu huyo ambapo msimu uliopita aliiwezesha kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kushika nafasi ya Pili katika Ligi kuu msimu uliopita.
Klabu hiyo inao wachezaji kadhaa wa Kulipwa kutoka nchi za Ivory Coast, Kenya na Uganda. Kuachia ngazi kwa kocha huyo kunaelezwa kuwa kumekuwa kwa mkakati ili kusiathiri mwenendo wa timu hususan wakati ligi ikiendelea na sasa kutaiwezesha Azam FC Kutafuta kocha mwingine hususan wakati huu ambapo ligi imefikia mapumziko.
KATIBU MKUU MSAIDIZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO, PROF. ELISANTE OLE GABRIEL, LEO ALITEMBELEA CHUO CHA FUTURE WORLD VOCATIONAL KILICHOPO ULONGONI 'A' GONGO LAMBOTO.
CHUO HICHO KINAFADHILIWA NA SHIRIKA LA PLAN INTERNATIONAL PAMOJA NA SERIKALI YA CANADA.

 Pro. Elisante ole Gabriel akizungumza jambo huku akimuonyesha mratibu wa fedha wa Plan International, Stella Tungaraza (kulia), wakati akizungumza na wanachuo wa Future World leo asubuhi.
 Wanachuo wa Future World wakimsikiliza kwa makini Prof. Gabriel.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Plan International ni miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo.
 Prof.Gabriel akisisitiza jambo.
 Prof. Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi na wanachuo wa Future World leo chuoni hapo.
Simon Ndembeka (shati nyekundu) mmoja wa maafisa wa Plan International akiwa pamoja na katibu msaidizi, Prof.Gabriel wakionyesha ishara ya mshikamano na baadhi ya wanachuo wa Future World kilichopo Ulongoni A Gondo lamboto. (Picha zote: Daniel Mkate)

Jumanne, 5 Novemba 2013

MENDE: TUMEWAPIGA M23 KAZI IMEMALIZIKA


Lambert Mende Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema majeshi yake kwa kushirikiana na kile kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupambana na waasi wa M23 kimewapiga waasi hao katika ngome yao ya mwisho.
Msemaji wa Serikali, Lambert Mende ameiambia BBC kuwa wapiganaji waliobaki wa M23 wanaweza wakawa wamekimbia, wamevuka mpaka au wamejisalimisha.
Mende amesema kikosi maalum cha majeshi ya nchi hiyo kimeharibu silaha za waasi hao usiku kucha na inasadikiwa kiongozi wa kijeshi wa kundi hilo la M23, Sultani Makenga ni miongoni mwa waliovuka mpaka na kuingia Rwanda au Uganda.
Wakati huo huo, viongozi wa nchi za SADC wanaokutana nchini Afrika Kusini wamezungumzia mgogoro wa Jumhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwataka viongozi wa kundi la waasi wa M23 kutangaza kusimamisha mapigano.
Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo imesema kama waasi hao watachukua hatua hiyo mkataba wa amani unaweza kusainiwa ndani ya siku tano zijazo.

CHANZO: BBC

Jumatano, 23 Oktoba 2013

UVAMIZI KANISANI: MMOJA AUWAWA WAWILI WAJERUHIWA VIBAYA

UVAMIZI KANISANI: MMOJA AUWAWA WAWILI WAJERUHIWA VIBAYA..!


 
Wananchi wakiwa wakitafakari nje ya jengo la Kanisa la Gilgal Christian Centre lililopo Pasiansi Ilemela jijini Mwanza.
 ----------
Mtu mmoja ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia shambulizi lililofanywa na kundi la watu wasiofahamika usiku wa
kuamkia jana  katika kanisa la Gilgal Christian Worship Centre lililopo eneo la Pasiansi wilaya ya Ilemela jijini Mwanza.
Tukio hilo lililotokea majira ya saa saba usiku linamtaja Elia Lunyamila (35) ambaye ni mlinzi  na ni  mwenyekiti wa vijana wa kanisa kuuawa akiwa amejumuika kwenye ibada na waumini wengine Alex Msakuzi na Tumsifu Pungu ambao hali zao zinatajwa kuwa taabani wakipatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kukatwakatwa mapanga sehemu mbalimbali za miili  yao. 
Askofu wa kanisa hilo Eliabu Sentoz amelaani tukio hilo akilitaja kuwa ni la kinyama kwani limefanyika sehemu ya ibada akiwataka wananchi kuungana pamoja kulisaidia jeshi la polisi katika kutoa taarifa kuwabaini wahusika wa shambulio  hilo na akaiomba serikali kuongeza nguvu kukabiriana na wahalifu hao.
Kamanda wa polisi mkoa wa  Mwanza , Ernest Mangu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mpaka sasa hakuna taarifa za kuibiwa kwa kitu chochote ndani ya kanisa, hali ambayo inalifanya tukio hilo kuwa na maswali mengi likihofiwa kufananishwa na yale ya uchomaji moto Makanisa.
Waumini wakitafakari tukio hilo la uvamizi lililosababisha taharuki kwa wakazi wa jiji la Mwanza.
 
 
Ndugu na majirani pamoja na waumini waliomfahamu marehemu Elia Lunyamila aliyeuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa marehemu kuomboleza
Askofu wa kanisa la Gilgal Christian Centre Eliabu Sentozi.
 
Chanzo: Masai Nyotambofu

SHAMBA LINAUZWA

SHAMBA LINAUZWA

LIPO KISANGA KISARAWE MBELE YA KIWANDA CHA SIMENTI.
UKUBWA NI EKARI MOJA KASORO KIDOGO.
BEI SH.MILIONI 6 (MAELEWANO YAPO)
LIPO JIRANI NA BARABARA LINA MAZAO MBALIMBALI
KAMA MAFENESI, MACHUNGWA, MACHENZA NA MITI YA MINAZI

WASILIANA KWA 0655 006971 AU 0755 006970
EMAIL: mkatedaniel@gmail.com

Jumatatu, 14 Oktoba 2013

KAMATI YA RUFANI YA MAADILI YA TFF YAFANYA MAPITIO

Msemaji wa TFF, Boniface Wambura

Kamati ya Rufani ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana jana (Oktoba 13 mwaka huu) kusikiliza maombi ya mapitio (revision) na mwongozo ya uamuzi wa Kamati ya Maadili.

Sekretarieti ya TFF iliwasilisha maombi ya mapitio kwa Kamati hiyo ya juu kabisa ya masuala ya maadili kutokana na ugumu wa utekelezaji wa uamuzi wa Kamati ya Maadili juu ya mashauri nane yaliyowasilishwa mbele yake.

Kamati ya Rufani ya Maadili itaendelea na kikao chake kesho (Oktoba 15 mwaka huu), na baadaye itakutana na waandishi wa habari (saa 10 jioni) kwa ajili ya kutangaza uamuzi wake juu ya mwongozo ulioombwa na Sekretarieti ya TFF.

KIONGOZI WA MWENGE AFUNGUA KITUO CHA IDYDCC
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Juma Ali Amir amefungua kituo cha kwanza cha Football for Hope kilicho mkoani Iringa kwa kuwataka wananchi kukituia vizuri ili wanufaike na huruma za kijamii zinazotolewa na taasisi ya IDYDC pamoja na kuendeleza mpira wa miguu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho jana (Oktoba 13 mwaka huu), kiongozi huyo amesema taasisi ya IDYDC (Iringa Development of Youth, Disabled and Child Care) wamefanya vizuri kuamua kutumia mpira wa miguu kusaidia jamii kwa kuelimisha juu ya mambo mbalimbali kama ugonjwa wa ukimwi, kusaidia walemavu, haki za watoto na afya ya jamii.
Naye Mwakilishi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Patrick Onyango amesema amefurahishwa na kukamilika kwa kituo ambacho kitasaidia jamii.
Amesema idadi kubwa ya watu waliofika kwenye uzinduzi huo inadhihirisha ni kiasi gani kituo hicho kitakuwa na matokeo mazuri kwa jamii.
Onyango alisema hicho ni kituo cha 14 kukamilika kati ya 20 vinavyojengwa barani Afrika ikiwa ni mpango wa FIFA kurudisha kwa jamii mafanikio iliyopata kwenye fainali za kwanza za Kombe la Dunia barani Afrika.

Kituo hicho kina uwanja mdogo wa mita 20 kwa 40 uliowekwa nyasi bandia, jengo lenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya semina, chumba cha kupimia ukimwi, chumba cha ushauri nasaha, maktaba na ofisi.
Zaidi ya dola 270,000 za Marekani zimetumika kukamilisha ujenzi wa kituo hicho kilicho eneo la Mtwivila, Iringa mjini.

KESSY KUSIMAMIA MECHI YA KOMBE LA DUNIA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Mtanzania Lina Kessy kuwa kamishna wa mechi ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kwa wanawake chini ya umri wa miaka 20 kati ya Botswana na Afrika Kusini.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza itachezwa nchini Botswana kati ya Oktoba 25 na 27 mwaka huu. Waamuzi kutoka Zimbabwe ndiyo watakaochezesha mechi hiyo namba tisa.

Waamuzi hao wataongozwa na Pamela Majo atakayepuliza filimbi wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Rudo Nhananga, namba mbili ni Stellah Ruvinga na mezani atakuwepo Tambudzi Tavengwa.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Mashauzi kutambulisha mpya Idd el Hajj Da' West Tabata

Bendi ya taarabu ya Mashauzi Classic kesho itatambulisha nyimbo zao mpyakwenye onyesho maalum ya kusherehekea sikukuu ya Idd el Hajj katika ukumbi
wa Dar West Park, Tabata.
Onyesho hilo ambalo linajulikana kama 'Usiku wa Isha Mashauzi', imeandaliwa
na Keen Arts na  Bob Entertainment chini ya udhamini wa kinywaji cha
Konyagi, Straika, Kwetu Mbambabay  na Saluti5.
Isha
Mratibu wa onyesho hilo, Joseph Kapinga amesema kuwa onyesho litakuwa la
kipekee na maalum kwa kusherehekea sikukuu ya Idd El Hajj.
Amesema katika onyesho hilo, Mashauzi atatambulisha albamu yake mpya
ijulikanayo kama "Asiyekujua Hakuthamini" ambayo ina nyimbo kama "Mimi Bonge
la Bwana," utunzi wake Hashim Said, "Ropokeni Yanayoyahusu" ( Saida
Ramadhani) na "Haya ni Mapenzi Tu" (Zubeda Malik).
Zawadi mbalimabli zitatolewa kwa mashabiki wa bendi hiyo inayojulikana kama
Wakali wa Kujiachia.
"Tumeandaa zawadi mbalimbali kwa mashabiki wetu. Pia bendi ya Mashauzi
Classic watatumia onyesho hilo kutambulisha nyimbo zao mpya," Kapinga
alisema.
"Mashauzi Classic watapiga albamu zao zote. Matumaini yetu ni kuwa watu
watapata burudani ya kutosha kuliko siku zingine zote," alisema Kapinga.
Nyimbo zingine zitakazopigwa ni  "Viwavijeshi" (Issa Ramadhani), "Sitasahau
Yaliyonikuta" (Abdul Malik), "La Mungu Halima Mwamuzi" (Zubeda Malik) na
"Sijamuona Kati Yenu" (Rukia Juma).
Naye mkurugenzi wa bendi hiyo, Isha Mashauzi, alisema kuwa onyesho la Da
West litakuwa la kihistoria na kutaka watu wajitokeze kwa wingi ili historia
isiwapite.
"Kwa kweli bendi iko fiti," alisema Mashauzi.

Ijumaa, 27 Septemba 2013

Wakuu wa usalama kuhojiwa Kenya

Sehemu ya jengo la Westgate iliyoporomoka
Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.
Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.

Walipuuza onyo?

Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

source: bbc

Alhamisi, 19 Septemba 2013

GOLI 6 ZA SIMBA ZAWAINGIZIA SH.MIL.13.8




MIL 58/- ZAPATIKANA MECHI YA SIMBA, MGAMBO
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

MIKATABA YA MAKOCHA VPL, FDL YATAKIWA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)