http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo

Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594

Usilikose kila Jumapili

Jumamosi, 10 Agosti 2013

SHEHE PONDA AJERUHIWA NA POLISI MOROGORO

Habari zilizo tufikia hivi punde katika meza yetu ya habari ya Father Kidevu Blog, zinapasha kuwa Sheikh Ponda Issa Ponda anadaiwa kujeruhiwa na Polisi muda mfupi baada ya kumaliza mhadhara wake Mjini Morogoro katika jaribio la kumkamata.

Taarifa kutoka eeo la tukio zinapasha kuwa Sheikh Ponda amejeruhiwa na bomu la machozi lililoplipuliwa katika gari lake wakati wa jaribio hilo la kumkamata jioni ya leo na kuzua mtafaruku mkali.

Aidha taarifa hizo zinasema mara baada ya tukio hilo baadhi ya Mashekh walimshusha katika gari lake na kumpakia katika Pikipiki na kumkimbiza Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu lakini ghafla walibaini kuwa Polisi wanawafuatilia na kuamua kuingia hospitalini hapo na kutokea mlango wa uwani na kutokomea.


Mtoa taarifa wa Fadha Kidevu Blog mjini Mrogoro anapasha kuwa wakati Ponda akitoroshwa mikononi mwa Polisi mlango wa uwani Polisi walitinga Hospitalini humo kufanya msako wa Shekh huyo ambaye amekuwa akileta kizazaa zaa kutoka na mawaidha yake na msimamo wake wa utetezi wa mali za Waislamu nchini.
Father Kidevu Blog itakupa taarifa kamili ya tukio hilo wakati wowote kuanzia sasa endelea kuifuatilia.