JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI
YA TAIFA YA UKAGUZI
TAARIFA KWA UMMA NA
VYOMBO VYA HABARI
Ufafanuzi wa Taarifa
Kuhusu Hali ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) zilizotolewa
kwenye baadhi ya vyombo vya Habari siku ya Ijumaa tarehe 12 Aprili 2013
kutokana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
iliyotolewa Bungeni.
1. UTANGULIZI
Siku
ya Ijumaa ya tarehe 12 Aprili 2013 baadhi ya vyombo vya Habari viliandika juu
ya taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali aliyoitoa Bungeni
tarehe 11 Aprili, 2013 isivyo sahihi zinazohusu Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi
wa Umma (PSPF) kama ifuatavyo:
v Kuwa Mfuko umepata
hasara ya Shilingi trilioni 6.487 na hali yake kifedha ni mbaya.
v Mfuko umekuwa ukitoa
mikopo bila ya kutoza riba.
2. UFAFANUZI
v Kuwa Mfuko umepata
hasara ya Shilingi trilioni 6.487 na hali yake kifedha ni mbaya.
Ninapenda kufafanua kuwa taarifa yangu ilivyotafsiriwa na
baadhi ya vyombo vya habari kuwa Mfuko umepata hasara ya shilingi trilioni 6.487 siyo sahihi.
Taarifa sahihi ni kuwa kiasi hicho ni nakisi (acturial deficit)
ambayo imetokana na fedha ambazo ni malimbikizo ya mafao (accrued liabilities)
ya Watumishi wa Umma kabla ya mwezi Julai mwaka 1999. Nakisi ya malimbikizo
hayo yanatokana na tathimini iliyofanywa na mthamini (acturial valuer) M/s
Genesis Actuarial Solutions kampuni kutoka Afrika Kusini.
Ninapenda
kutoa ufafanuzi kuwa taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari kuwa kiasi
kilichotajwa ni nakisi ya malimbikizo ya mafao ya watumishi na sio hasara ya
upotevu wa fedha.
Hata
hivyo, katika mwaka wa fedha 2010/2011 Serikali ilikubali kuanza kurejesha
mafao yaliyolipwa awali kwa wafanyakazi waliostaafu kazi kuanzia mwaka 2004.
v Mfuko umekuwa ukitoa
mikopo bila ya kutoza riba.
Kuhusiana
na taarifa kuwa PSPF imekuwa ikitoa mikopo bila ya kutoza riba siyo sahihi.
Taarifa
sahihi ni kwamba kiasi cha fedha kilichoonyeshwa kwenye ripoti ni mikopo
(principal amount) ambayo haikujumuisha
riba na siyo kwamba mikopo hiyo haitozwi riba. Mikopo hiyo hutozwa riba na
adhabu hutolewa pindi inapocheleweshwa kurejeshwa na wakopaji.
Ni
imani yangu kuwa, waandishi wa habari wataendelea kuuhabarisha Umma wa Tanzania
juu ya ripoti zangu kwa usahihi na pale patakapokuwa hapaeleweki, naomba mje
ofisini kwangu kwa ufafanuzi.
Francis
Mwakapalila
K.n.y MDHIBITI NA
MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
|
|
http://www.mkcomputertweaks.com/mkgroup/fkbmksb.gifMatangazo
Tangaza nasi: mkatedaniel@gmail.com, +255 7666-00 69 70, +255 655-00 69 71, +255 787- 249594